• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAZIRI MCHENGERWA ARIDHISHWA NA MATUMIZI YA ZAIDI YA TRIL.11 ZILIZOTOLEWA NA SERIKALI KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI KIGOMA

Posted on: August 14th, 2024

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb)amesema ameridhishwa na matumizi ya Fedha zaidi ya Shilingi Tril.11 zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita kwa ajili ya kutekeleza miradi ya Maendeleo mkoani Kigoma.

Mhe. Mchengerwa ametoa kauli hiyo alipozungumza mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya Siku tatu mkoani Kigoma na kusisitiza kuwa pamoja na matumizi mazuri ya fedha hizo yapo maeneo hakuridhika na utekelezaji wa miradi kutokana na kukwamishwa na wasimamizi wa miradi hiyo jambo linalochangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha maendeleo ya wananchi.

Amesema katika maeneo yote aliyobaini baadhi ya watendaji wa Serikali kutumia kinyume na utaratibu fedha zinazotolewa na Serikali, ametoa maelekezo sambamba na kuchukua hatua dhidi ya watendaji walioshiriki kukwamisha miradi ya serikali.

‘’Tunakwenda kukutana na watendaji wenzangu walio chini ya wizara hii ili kuandaa Taarifa kamili kwa ajili ya kuchukua hatua katika maeneo yote ambayo watendaji hawakufanya vizuri kwa sababu za kushindwa kuwajibika’’ amesema Waziri.

‘’Nasisitiza hata kama mtumishi amehitimisha muda wake wa utumishi serikalini, amehamishwa au uteuzi wake umetenguliwa tutamrejesha hapa ili aweze kujibu makosa yake iwapo tutathibitisha kuwa mtumishi huyo alishiriki kupokea rushwa,  kusababisha ubadhirifu au aina yoyote ya upotevu wa fedha za serikali hatutosita kuchukua hatua’’amesisitiza Mhe. Mchengerwa.

Mchengerwa ametoa wito kwa viongozi wote wa serikali kukumbuka wao ni watumishi wa wananchi, hivyo watumie nafasi zao kuwatumika watanzania. Ukiwa waziri, Mkuu wa Mkoa, mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi nk, jitahidi kuwatumikia wananchi ili uweze kuacha alama kwa unaowatumikia na Taifa kwa ujumla.

Awali waziri huyo amekagua jengo la Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Uvinza na kuielekeza TAKUKURU kufanya uchunguzi kuhusiana na ujenzi wa jengo la ofisi hiyo kutokana na waziri huyo kubaini baadhi ya kazi zilizofanyika katika ujenzi wa jengo hilo kutozingatia miongozo ya serikali na kukosa ubora.

Aidha amemuelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha ndani ya Siku mbili kuanzia Agosti 14, 2024, jengo hilo linaunganishwa kwenye mfumo wa Umeme ili kurahisisha utendaji kazi wa watumishi wanaotumia ofisi hiyo.

Akiwa katika shule ya sekondari ya Uvinza Wasichana, Mhe. Mchengerwa amemuelekeza mhandisi wa Wilaya hiyo kuhakikisha huduma ya Umeme inafika kwenye mabweni yote ya shule hiyo.

Aidha Mchengerwa amepata fursa ya kuzungumza na wanafunzi wa shule hiyo na kusisitiza kuwa Mhe. Rais anaguswa na changamoto ya upatikanaji wa elimu bora kwa watoto wa kike ndio maana akaanzisha utaratibu wa kujenga shule hizo ili kuweza kuwapa fursa wasichana kupata elimu bora.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa