• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

UJENZI KITUO CHA AFYA MAKERE WAFIKIA ASILIMIA 70

Posted on: August 27th, 2025

Wakazi wa kata ya Makere wilayani Kasulu mkoani Kigoma wameishukuru Serikali kwa kufanikisha ujenzi wa Kituo cha Afya wilayani humo hali itakayowaondolea adha ya muda mrefu ya ukosefu huduma za afya kwa ukaribu na kusababisha kwenda kutibiwa maeneo ya mbali huku baadhi yao wakipatiwa matibabu katika Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo wilayani humo.

Mradi huo unaotekelezwa na Serikali kwa Thamani ya Shilingi Bil 1.66 kupitia miradi ya nyongeza itokanayo na ujenzi  kwa barabara kwa kiwango cha lami Kabingo, Kasulu hadi Manyovu chini ya Ufadhili wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba 2025 ukihusisha ujenzi wa jengo la Utawala, wazazi, upasuaji, Maabara, jengo la kuhifadhia maiti, ufuaji pamoja na jengo la makazi ya mtumishi.

Method Erick ambaye ni mkazi wa kata hiyo amesema mara nyingi zinapotokea changamoto za kiafya kwa wakazi katika eneo hilo na jirani wamekuwa wakitegemea kituo cha Afya kilichopo katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu ambapo wamekuwa wakichelewa kupata huduma kutokana mchakato wa kupata vibali ili kuingia kambini humo jambo ambalo limekuwa likihatarisha maisha ya wagonjwa mahututi pamoja na  wanawake walio katika hatua ya kujifungua.

Peter Basilia Mkazi wakijiji cha Nyangwa kata ya Makere, amesema awali kwa sasa tegemeo kuu la matibabu katika kata hiyo ni Zahanati ya kijiji pekee huku eneo hilo likiwa na idadi kubwa ya wakazi, hali inayosababisha kituo hicho cha kutolea huduma ya afya kuwa na foleni kubwa ya wagonjwa huku kikiwa na idadi ndogo ya watendaji na vifaa visivyokidhi mahitaji ya kitabibu.

Amesisitiza kuwa, kituo hicho kitapunguza au kuwaepusha kabisa na  gharama za kusafirisha wagonjwa ili  kuwafikisha katika  vituo vingine vya kutolea huduma za afya ikiwemo Hospitali za Wilaya na mji Kasulu au Hospitali ya Rufaa ya Kabanga iliyopo wilayani humo.

Naye Mganga Mkuu Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Dkt. Joseph Tubeti amesema mradi utakapokamilika utaongeza fursa za upatikanaji huduma za afya za msingi, upasuaji kwa mama watakaopata changamoto ya uzazi pingamizi pamoja na huduma ya kuhifadhi miili inapotokea vifo.

Amesema kata ya makere inakadiriwa kuwa na wakazi Zaidi ya Sitini elfu hivyo uwepo wa huduma hiyo utapunguza mzigo kwa vituo jirani vya kutolea huduma za afya. Aidha amesisitiza kuwa kwa sasa hali ya upatikanaji vifaa  tiba imezidi kuimarika hali inayochangia kwa kiasi kikubwa uwepo wa ufanisi katika kukabiliana na maradhi wilayani humo.

Aidha Dkt. Tubeti ametoa wito kwa wananchi kutumia fursa ya uwepo wa ongezeko la vituo vya kutolea huduma za Afya kuejenga tabia ya kujitokeza na kupima afya zao mara kwa mara ili kuepukana na matibabu ya muda mrefu yatokanayo na usugu wa maradhi.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • UJENZI KITUO CHA AFYA MAKERE WAFIKIA ASILIMIA 70

    August 27, 2025
  • UJENZI KITUO CHA AFYA RUKOMA KUWAONDOLEA ADHA WAKAZI KUFUATA HUDUMA ZA AFYA ZAIDI YA KM 10

    August 25, 2025
  • MRADI WA AFYA HATUA KUONGEZA KASI MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI MANISPAA YA KIGOMA UJIJI

    August 18, 2025
  • MRADI WA AFYA HATUA KUONGEZA KASI MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI MANISPAA YA KIGOMA UJIJI

    August 18, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa