• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC SIRRO AKABIDHI VITENDEA KAZI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KIGOMA

Posted on: October 24th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amekabidhi magari manne yaliyotolewa na Serikali kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kigoma huku akitoa wito kwa wananchi kutoa taarifa kwa wakati  kuhusu uwepo wa matukio ya ajali za moto na matukio mengine yanayoshughulikiwa na jeshi hilo.

Amesema, mara baada ya kupokea vitendea kazi hivyo, Jeshi  hilo linapaswa  kuongeza ufanisi kiutendaji kazi huku akisisitiza utunzaji wa magari na vifaa vingine vilivyopokelewa ili viweze kufanya kazi kwa muda mrefu.

"Pamoja na ukosefu wa vitendea kazi vya kutosha, Jeshi hili limeendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kupata mafanikio makubwa kila ilipohitajika kufanya hivyo. Nichukue fursa hii kuwapongezeni kwa kazi nzuri mnazofanya" amesema Sirro.

Aidha Balozi Sirro ameishukuru serikali kwa kuwezesha upatikanaji  wa vitendea kazi hivyo, jambo litakaloimarisha utendaji kazi wa jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani hapa.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa ametoa rai kwa Jeshi hilo kutumia vyombo hivyo kwa lengo la kuleta mapinduzi katika eneo lao la utendaji kazi wao.

Amemuhakikishia mkuu wa mkoa kuwa, kwa kushirikiana na uongozi wa jeshi hilo watahakikisha nyenzo hizo zinatumika kwa kuzingatia malengo ya serikali.

Awali akitoa taarifa ya mapokezi ya vifaa hivyo, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji  Mkoa wa Kigoma Michael Maganga, amesema vitendea kazi walivyopokea  ni pamoja na mtambo wa kisasa wa kuzima moto, gari la kubeba maji, gari la operesheni na gari la wagonjwa.

Ametoa wito kwa wananchi mkoani hapa kuendelea kushirikiana na jeshi hilo kwa kutoa taarifa mapema ili liweze kufika maeneo ya matukio kwa  wakati jambo litakalofanikisha kupunguza athari za majanga.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC SIRRO AKABIDHI VITENDEA KAZI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI KIGOMA

    October 24, 2025
  • UJENZI WA MITARO SABA YA MAJI KUNUSURU KAYA ZAIDI YA 300 KIGOMA UJIJI

    October 16, 2025
  • SIRRO AKUTANA NA MWAKILISHI WA MKANDARASI WA UJENZI SGR UVINZA-MSONGATI BURUNDI

    September 24, 2025
  • RC SIRRO AAGIZA KUFANYIKA UPYA KWA TATHMINI SHAMBA LA MWEKEZAJI NA 206 LUGUFU UVINZA

    September 02, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa