• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAZIRI MCHENGERWA AAGIZA TARURA KUWEKA TAA KWENYE BARABARA WANAZOJENGA MKOANI KIGOMA

Posted on: August 14th, 2024

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) amememuelekeza Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini nchini  TARURA  Mkoa wa Kigoma kuweka taa katika barabara zote zinazojengwa na wakala huyo mkoani Kigoma ili kudumisha usalama nyakati za usiku sambamba na kupendezesha miji katika maeneo zilipo barabara hizo.

Mhe. Waziri Mchengerwa ametoa maelekezo hayo alipokagua mradi wa ujenzi wa barabara iliyojengwa kwa kiwango cha lami Km. 1.1 kutoka Ujenzi hadi GTZ na Kiganamo hadi Bogwe katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu, akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani hapa.

Amesema Mhe.Rais Dkt. Samia amelenga kuendelea kuimarisha miundombinu ya barabara mkoani Kigoma ili kuvutia wawekezaji na wafanyabiashara kupitia sekta hiyo muhimu ya uchukuzi sambamba na kuboresha mazingira ya miji katika mkoa huo na Tanzania kwa ujumla.

Ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha lami nyepesi umegharimu kiasi cha Shilingi Mil. 950, fedha kutoka serikali kuu na kukamilika kwake kumetajwa kuwaondolea adha ya ubovu wa barabara wakazi wa mji huo na kuzifanya zipitike kwa wepesi nyakati za masika na kiangazi.

Awali akiwa waziri huyo ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Mwami Ntale kilichopo katika Halmashauri hiyo na kumuagiza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo kumbadilishia Kituo cha Kazi Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Kasulu Dkt.Peter Janga kutokana na kutoridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho.

‘’Haiwezekani kituo kifunguliwe na kukosa Samani kwa kipindi cha zaidi ya Mwaka, huku kikiwa hakina Umeme na majengo kutotosheleza, hii haikubaliki na nnakuagiza Katibu Mkuu kumbadilishi kituo cha kazi sambamba na kuitaka TAKUKURU kufika hapa na kuanza uchunguzi wa ujenzi wa mradi huu’’amesema mchengerwa.

Katika hatua nyingine Waziri Mchengerwa ameiagiza TAKUKURU kufanya uchunguzi katika Shule ya Sekondari Nyumbigwa Mpya kupitia Program ya P4R kwa kiasi cha Shilingi Bil. 1 na fedha hizo kumalizika huku baadhi ya miundombinu ya Shule ujenzi wake kutokuwa umekamilika.

Kupitia ziara hiyo, Waziri Mchengerwa amesikiliza na kupokea kero za wananchi katika kata ya Kagerankanda ikiwemo uwepo wa changamoto ya uwepo wa migogoro ya ardhi, kata hiyo kutokuwa na diwani tangu mwaka 2021 sambamba na ombi la kupandishwa hadhi kwa shule ya sekondari kimenyi hadi kufikia kidato cha Sita.

Akitoalea ufafanuzi jero hizo za wananchi, Waziri huyo ameahidi kupeleka wataalam kutoka Wizara hiyo wanaoshughulikia masuala ya Elimu ili kuona kama Shule hiyo ya Sekondari ya Kimenyi inakidhi vigezo vya kupandishwa hadhi hadi kutoa Elimu ya Kidato cha Sita.

 Sambamba na hilo, waziri Mchengerwa ameahidi kukutana na Diwani wa Kata hiyo aliyesimamishwa kwa changamoto za masuala ya uraia ili kufahamu kiwango cha utatuzi wa changamoto zake ili aweze kurudi kuwatumikia wananchi.

Kuhusu suala la migogoro ya ardhi, Mchengerwa ameahidi kurudi katia kata hiyo ndani ya kipindi cha Siku 30 akiwa na Waziri mwenye dhamana ya ardhi ili kutatua na kuzitolea maamuzi changamoto ambazo wananchi hao wanankutana nazo kupitia sekta hiyo.




Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa