• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAZIRI MASAUNI AHIMIZA UREJEAJIWA HIYARI KWA WAKIMBIZI WA BURUNDI

Posted on: June 6th, 2024

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI. MHANDISI HAMAD MASAUNI AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI MARA BAADA YA KUFUNGA KIKAO CHA PANDE MBILI KILICHOWAHUSISHA WATAALAM KUTOKA NCHI ZA TANZANIA NA BURUNDI KWA  AJILI YA KUJADILI NA KUWEKA MIKAKATI YA PAMOJA  YA UTEKELEZAJI WA ZOEZI LA UREJEAJI WA WAKIMBIZI KUTOKA NCHINI BURUNDI.

WAZIRI MASAUNI(KATIKATI) AKIFUATILIA  JAMBO WAKATI KIKAO HICHO KIKIENDELEA. WA KWANZA KUSHOTO NI MKUU WA MKOA WA KIGOMA THOBIAS ANDENGENYE, NA WATATU KULIA NI MWAKILISHI KUTOKA SERIKALI YA BURUNDI THEOPHILE NDARUFATIYE.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema Serikali ya Tanzania itaendelea kutumia utaratibu wa hamasa katika kuhakikisha wakimbizi kutoka Burundi wanarejea nchini humo kutokana na kuimarika kwa hali ya Amani na utulivu.

Waziri Masauni ametoa Kauli hiyo alipozungumza wakati akifunga Kikao cha wataalam walioziwakilisha nchi za Tanzania na Burundi, kilichofanyika mkoani hapa kwa lengo la kujadili urejeaji wa wakimbizi hao na kusisitiza kuwa jitihada hizo zisitafsiriwe kuwa ni chuki bali ni dhamira ya serikali zote mbili kuwataka wakimbizi hao kurejea nchini humo kwa jili ya kujenga nchi yao.

Amesema lengo la serikali hizo mbili ni kuhakikisha linapatikana suluhisho la kudumu ili wakimbizi waweze kurejea nchini Burundi kwa hadhi, usalama na upendo kupitia utaratibu wa Hamasa utakaowawezesha kupata fursa za kifedha sambamba na vifaa vitakavyowasaidia kuanza maisha nchini humo.

‘‘Kwa sasa tupo katika kipindi cha hamasa kwa ajili ya urejeaji wa hiyari mpaka itakapofika Mwishoni mwa mwezi Desemba 2024, baada ya hapo mpango huo usipokamilika,  wakimbizi hao watakuwa wamepoteza hadhi ya ukimbizi hivyo litafuata zoezi la  kuwahoji na kufahamu sababu za kila mmoja kuendelea kuwepo nchini ili kuona  kama zitaendelea kumpa sifa ya kuwa mkimbizi’’  amefafanua Mhandisi Masauni.

Waziri huyo amesisitiza kuwa, Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kushughulikia masuala yote yanayowahusu  wakimbizi kwa kuheshimu na kuzingatia Sheria na Mikataba yote iliyopo kikanuni ili kuweza kuwarudisha wakimbizi hao nchini mwao kwa heshima na staha.

Aidha Waziri Masauni amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwa kufanya jitihada kubwa zilizosababisha mkoa wa Kigoma kuendelea kuwa katika hali ya usalama, Amani na utulivu.

Upande wake Mwakilishi wa Serikali ya Burundi Theophile Ndarufatiye amesema idadi ya wakimbizi wanaorejea nchini humo ni ndogo sana jambo lililowasukuma kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuendelea kuweka mikakati ya pamoja kuhakikisha kasi ya urejeaji kwa hiyari inaongezeka.

‘’Tangu mwaka 2017 hadi kufikia 2024 jumla ya wakimbizi 1,070,607 wamerejea nchini Burundi ambapo kwa mwaka 2024 hadi kufikia Mei 31, jumla ya wakimbizi 5,709 wamerejea huku zaidi ya wakimbizi laki moja bado wanaendelea kupatiwa hifadhi katika kambi za Nyarugusu na Nduta’’ amesema Ndarufatiye.

Mwakilishi huyo ameishukuru serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuwakarimu raia hao wa nchi hiyo huku akisisitiza kuwa wakimbizi watakaorejea kwa hiyari nchini humo kupitia mpango wa hamasa watapatiwa kiasi cha fedha kwa ajili ya kujikimu, huduma za vyeti vya uraia na ndoa, watoto wao kupelekwa shule, kupatiwa makazi, vifaa vya ujenzi pamoja na huduma nyinginezo muhimu za kijamii.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa