• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAZIRI JAFO AIDHINISHA UENDELEZAJI MAKAZI MTAA WA SANGANIGWA MANISPAA YA KIGOMA-UJIJI

Posted on: September 9th, 2022

Waziri Dkt. Selemani Jafo akiwa na viongozi wa Serikali Mkoa wa Kigoma mara baada ya kukagua eneo la Mlima Mlole katika Mtaa wa Sanganigwa Manispaa ya Kigoma-Ujiji ambalo hapo awali Serikali ilisitisha uendelezaji wa Makazi pamoja na shughuli nyinginezo za kibinaadamu  kutokana na uwepo wa atahari kubwa za kimazingira.Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Gabriel Msovela (wakwanza kushoto) Mkuu  wa Mkoa wa Kigoma CGF(Mst) Thobias Andengenye pamoja na Waziri Dkt. Selemani Jafo wakifurahia jambo na wananchi (hawapo pichani) mara baada ya kumaliza kuzungumza na Wakazi wa Mtaa wa Sanganigwa na kuwaruhusu kuendelea na shughuli za uendelezaji wa makazi katika eneo la Mlima Mlole.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Dkt. Selemani Jafo, ameidhinisha uendelezaji wa Makazi katika Eneo la Mlima Mlole Kata ya Sanganigwa, Manispaa ya Kigoma-Ujiji mkoani Kigoma ambapo awali Serikali ilisitisha shughuli hizo ili kuchunguza iwapo zingeweza kuleta Athari  za kimazingira katika Bandari ya Kigoma.

Waziri Jafo amesema Serikali kwa kutumia Wataalam wa Bandari pamoja na Mazingira wamejiridhisha kutowepo kwa Athari hizo kwa sasa kutokana na uimarishwaji wa kuta za mto Rubengela  uliokuwa ukisababisha mmomonyoko wa Ardhi nyakati za mvua katika eneo hilo na kupelekea tope na mchanga mwingi kuingia eneo la bandari na kuathiri ufanisi katika utendaji kazi.

Amri ya zuio la kuendeleza makazi ilitolewa na mamlaka ya usimamizi wa Bandari mkoani Kigoma Mwaka 2009 ambapo wakazi wa eneo hilo walitakiwa kusitisha ujenzi wa nyumba pamoja na shughuli nyingine za kibinaadamu  ili kusubiri kufanyika kwa utafiti ambao ulisababisha Serikali kuja na jibu la ujenzi wa kingo za Mto huo hali iliyopunguza mmomonyoko wa Ardhi katika eneo hilo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Uzimamoto na Uokoaji, Mhe.Thobiasi Andengenye amemshukuri Waziri Jafo kwa kutoa maamuzi yaliyowagusa wakazi wa eneo hilo na wanakigoma kwa ujumla.

‘’Nawaagiza wataalam watakaohusika na utoaji wa vibali kwa ajili ya uendelezaji wa makazi katika eneno hili kuhakikisha wanatekeleza zoezi hili kwa uadilifu mkubwa na utoaji wa vibali usizidi siku Thelathini tangu siku ya kupokea maombi ya vibali hivyo.’’ Amesema Andengenye.

Amesisitiza kuwa wananchi watakaokutana na kadhia yoyote wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo, wasisite kutoa taarifa kwa uongozi wa juu ili kuchukua hatua kwa yeyote atakayeonekana kukwamisha utendaji kazi.

Baadhi ya Wananchi wenye majengo pamoja na viwanja katika eneo hilo, hawakusita kumshukuru Waziri Jafo pamoja na Uongozi wa Mkoa kwa kufikia maamuzi hayo yenye tija kwao na Jamii ya wanakigoma kwa ujumla.

‘’Sula hili limeleta sintofahamu kwetu kwa zaidi ya miaka kumi na tatu, hivyo maamuzi yaliyofikiwa yametugusa na kutufanya tuwe na Amani kwa sababu baadhi yetu walilazimika kuishi katika nyumba za kupanga wakati wakisubiri hatma ya suala hili’’ alisema Rajabu Maboza Mkazi wa  kata ya Sanganigwa Manispaa ya Kigoma-Ujiji.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa