• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAZIRI DKT. CHANA AZINDUA MPANGO WA USAJILI NA UTOAJI WA VYETI VYA KUZALIWA KIGOMA

Posted on: October 3rd, 2023

NA. GRADNESS KUSAGA-KIGOMA

Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali imedhamiria kutekeleza mpango wa kudumu wa usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa bure ili kuhakikisha kila mtoto anayezaliwa anapata haki hiyo.

Akizungumza kwenye Hafla ya uzinduzi wa Mpango wa Usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye Umri chini ya miaka mitano mkoani Kigoma iliyofanyika katika viwanja vya Mwanga Centre, Waziri Dkt. Chana amesema cheti cha kuzaliwa ni haki ya Msingi kwa kila mtoto anayezaliwa ndani ya mipaka ya Tanzania.

Amesema Serikali imeandaa mpango huo ikilenga kuhakikisha huduma ya upatikanaji wa vyeti hivyo, inayotolewa karibu na makazi ya wananchi kupitia Ofisi za watedaji wa kata na vituo vya kutolea Huduma za Afya vilivyopo katika maeneo yao ili kuwapunguzia upotevu wa muda na fedha kwa ajili ya kufuata huduma hiyo katika makao makuu ya wilaya.

Amefafanua kuwa, Tangu kuzinduliwa kwa mpango huo Juni 2023, zaidi ya watoto Mil. 8.6 wamesajiliwa na kupatiwa  vyeti vya kuzaliwa katika mikoa 24 ambayo mpango huo unaendelea kutekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na  wadau wake.

‘’Niendelee kuwakumbusha kinamama wajawazito kujifungua kwenye vituo vya Afya ili mtoto anapozaliwa aweze kupata cheti chake cha kuzaliwa na mzazi unapaswa kukichukua kwa kuwa ni haki ya mtoto aliyezaliwa’’ amesisitiza Dkt. Chana.

Aidha mpango huo mkoani Kigoma unawalenga jumla ya watoto 393,216 wenye umri chini ya Miaka mitano  ambao wanatarajiwa kusajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa.

Awali akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mkuu wa wilaya ya Kigoma Salum Kalli amesema mkoa unajumla ya vituo 443 kwa ajili ya ya kutolea huduma ya usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa.

Amesema kuwa wataalam watakaohusika na utekelezaji na usimamizi wa zoezi hilo wamejipanga kukabiliana na changamoto za uwepo wa Raia wa nchi jirani kwa kubainisha uhalisia wa taarifa zao.

Pia Kalli amewakumbusha wazazi wajibu wa kutunza vyeti hivyo kwa kuwa ni kumbukumbu muhimu za maisha ya watoto wao ili waweze kuwakabidhi pale watakapofikia umri wa kutosha kutambua umuhimu wa nyaraka hizo.

Upande wake Mwakilishi wa Serikali ya Canada ambao ni wafadhili wa mpango huo Bronwin Crude amesema nchi yake inajivunia kuunga mkono utekelezaji wa mpango huo kwa sababu usajili wa vizazi ni haki ya msingi kwa ajili ya kupanga mipango ya Maendelo ya nchi.

Aidha amesisitiza kuwa mfumo wa usajili wa vizazi unazingatia jinsia zote ili kuhakikisha haki za watoto zinalindwa kwa mustakabali wa maendeleo ya Taifa katika Siku zijazo.     

      

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa