• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WATUMISIHI WA AFYA MKOANI KIGOMA WATAKIWA KUFUATA MAADILI YA KAZI

Posted on: May 12th, 2017

Watumishi wa sekta ya Afya wametakiwa kuwa na nidhamu ya kazi na kuzingatia maadili ya tasnia yao wanapokuwa katika kutekeleza majukumu yao ikiwa pamoja na matumizi ya lugha nzuri, kuheshimiana na kuthaminiana.

Haya yameelezwa wakati wa ziara na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma wa Kigoma, Mhe. Brigedia Jenerali (mstaafu) Emanuel Maganga alipokuwa anazungumza na watumishi wa Hospitali ya Mkoa ya Rufaa –Maweni Mkoani Kigoma.

Alisema kuwa ili kuwa na maendeleo suala la afya za watu ni lazima lipewe umakini mkubwa, hii ni pamoja na kwanza watumishi kushirikiana wao kwa wao pamoja na wanaowahudumia “wasaidieni wananchi waeleimisheni pia masuala ya lishe kuepukana na udumavu pamoja na unyafuzi”.

Mhe. Maganga amewapongeza na kuwashukuru Wafanyakazi wote wa Hospitali ya Rufaa ya Maweni kwa kuwatumikia watanzania katika suala zima la afya. Ameendelea kuwahimiaza wachape kazi, licha ya changamoto wanazozikabili Serikali ya awamu ya tano inatambua hayo na inayafanyia kazi yatakwisha kwa awamu.

Akisoma taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Mganga Mkuu wa Mkoa ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Afya Dkt Paul Chaote alieleza kuwa pamoja na kuwepo kwa Changamoto hospitali imejitahidi kuongeza ukusanyaji wa mapato kupitia fedha za uchangishaji (cost sharing) ambapo makusanyo kwa kutumia mfumo wa  kielektroniki yameimarika kutoka milioni 23,541,700 mwezi Julai 2016 hadi Shilingi Milioni 32,049,340 mwezi Machi 2017.

Dkt. Chaote ametaja pia upugufu wa watumishi ni changamoto inayoikabili. Hospitali inaupungufu wa watumishi 451 kati ya 681 wanaohitajika, alieleza kuwa kati ya mapungufu hayo kuna mapungufu ya Madaktari bingwa hali ambayo inachangia rufaa nyingi kutolewa ambazo zingeweza kufanyika haospitalini hapo. Hata hivyo ameishukuru Serikali kwani imeanza kuleta watumishi katika hospitali hiyo ambapo hivi karibuni wameripoti madaktari watatu.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa