• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WATUMISHI WA UMMA WAHIMIZWA UWAJIBIKAJI KUEPUKA HOJA ZA CAG

Posted on: June 21st, 2024

Watumishi wa Umma katika halmashauri za Mkoa wa Kigoma wametakiwa kuzingatia kanuni, taratibu na Sheria za matumizi ya Fedha za Umma ili kuepuka kusababisha hoja za ukaguzi wa Hesabu za Serikali katika Halmashauri hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye ametoa kauli hiyo alipozungumza na Madiwani kupitia Mikutano Maalum wa mabaraza ya Madiwani katika Halmashauri Wilaya ya Kigoma na Manispaa ya Kigoma Ujiji, kwa ajili ya kujadili hoja na Mapendekezo ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 uliofanyika Juni 21. 2024 katika Halmashauri hizo.

‘‘Ili kudhibiti hoja katika maeneo yenu mnatakiwa kuwasilisha nyaraka za matumizi yote ya fedha kwa wakati sambamba na kutoa ushirikiano wa karibu kwa wakaguzi wa ndani katika Halmashauri zenu’’ amesisitiza Andengenye.

Amesema lengo la mkoa ni kuhakikisha halmashauri zote ziwe zinashughulikia hoja zisizozidi tisa ifikapo mwaka 2025/2026 kutokana na mkoa kuanza kutekeleza mkakati wa kubaini na kudhibiti viashiria kabla havijawa hoja kamili.

Aidha amezitaka halmashauri hizo kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato ya ndani  sambamba na kutumia Asilimia Arobaini ya Mapato hayo kutekeleza miradi inayoonekana na kuwagusa wananchi moja kwa moja badala ya utekelezaji wa miradi ya kwenye makaratasi.

Sambamba na hilo, mkuu huyo wa mkoa amezielekeza halmashauri hizo kuhakikisha zinapima maeneo yote yanayomilikiwa na Taasisi za Umma na kuzipatia hati miliki ili kudhibiti wavamizi wanaosababisha ongezeko la kesi za migogoro ya ardhi.  

Aidha Mkuu wa mkoa ametoa wito kwa wakazi mkoani hapa kujitokeza na kushiriki katika zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura lililolenga kutoa fursa ya kuandikisha wapiga kura wapya, kurekebisha taarifa za wapiga kura sambamba na kuondoa taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za kuwemo katika orodha hiyo.

Upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema mkoa umejipanga kuongeza ushirikiano na wakaguzi wa ndani ili kupunguza idadi ya hoja hadi kufikia chini ya kumi kwa kila halmashauri kwa kila mwaka wa fedha.

Aidha amewaelekeza wakurugenzi kuhakikisha wanawasimamia wakuu wa Idara na Vitengo ili waweze  kujibu hoja zinazojitokeza kwa usahihi na kuzingatia muda kwa sababu majibu ya hoja hizo yapo  chini ya mamlaka yao.  

Katika hatua nyingine Katibu Tawala amewataka madiwani hao kuwa mabalozi wazuri katika kuhamasisha uchangiaji wa chakula shuleni ili wanafunzi waweze kupata chakula shuleni kwa lengo la kudhibiti mdondoko wa wanafunzi katika baadhi ya shule za Halmashauri mkoani hapa.

Kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji na wilaya ya Kigoma vijijini zimefanikiwa kupata hati safi ya ukaguzi wa Hesabu za Serikali.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa