• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WATUMISHI WA UMMA MKOANI KIGOMA WAHIMIZWA KUONGEZA USHIRIKIANO KATIKA UTENDAJI KAZI

Posted on: May 5th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewataka watumishi wa Umma mkoani hapa kuendelea kushirikiana ili kuleta matokeo chanya katika utendaji kazi wao kwa lengo la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Andengenye ametoa wito huo alipozungumza na watumishi katika Halmashauri ya Buhigwe aliposhiriki hafla fupi ya kuwapongeza wafanayakazi hodari kwa mwaka 2023/2024 waliotambuliwa na Halmashauri hiyo kupitia maadhimisho ya Mei Mosi 2024 yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Mji Kasulu.

Amewaeleza watumishi hao kuwa, ni vizuri kila mmoja akatambua na kutekeleza wajibu wake kuendana na miongozo ya kazi yake badala ya kusubiri kusukumwa na viongozi wake katika eneo la utendaji kazi.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amewataka viongozi wa watumishi wa Umma mkoani hapa kujenga tabia ya kutumia njia ya hamasa ili kuwapa motisha chanya watumishi hao badala ya kutumia  lugha za vitisho, jambo linalosababisha kushuka kwa ari ya utendaji kazi.

‘‘watu wakikosa ari ya kufanya kazi hujikuta wakihudhuria ofisini badala ya kufima maeneo hayo kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao, kutoakana na hofu ya kuachishwa kazi au vitisho kutoka kwa wasimamizi wao, jambo hili ni changamoto kubwa katika ofisi zetu’’ amesema Andengenye.

Kiongozi huyo amewataka watumishi mkoani hapa hususani waliopo katika Wilaya ya Buhigwe kutumia fursa ya uwepo wa rasilimali ardhi katika halmashauri hiyo kwa lengo la kuwekeza katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali  ili kujiimarisha kiuchumi.

Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Michael Ngayalina amewakumbusha watumishi hao kuendelea kuitumikia jamii  ili waweze kuacha alama.

Aidha amewapongeza watumishi wote wa halmshauri hiyo  kwa umoja walionao katika utekelezaji wa majukumu yao huku akiwataka kuongeza bidi katika utendaji kazi  na kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi na kuwaondolea kero zao.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo George Mbilinyi amesema kitendo cha kuwatambua watumishi hodari na kutoa pongezi katika hamashauri kinatoa motisha na chachu kwa watendaji wengine kuongeza bidi katika utendaji kazi wao ili kuyafikia malengo yaliyowekwa na kuwapa fursa ya kutambuliwa katika wakati ujao.

‘’Niwaombe watumishi wenzangu tuzidi kufanya kazi ili tuiletee wilaya ya Buhigwe matokeo ambayo Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anayatarajia tuyafikie katika kutatua changamoto za wakazi’’  amesisitiza Mbilinyi.

PICHA ZA PAMOJA  ZA WASHIRKI WAKIWA NA MGENI RASMI MHE. KAMISHNA MSTAAFU WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI THOBIAS ANDENGENYE.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC SIRRO AZINDUA ZOEZI LA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO KIMKOA

    July 03, 2025
  • JESHI LA UHAMIAJI KIGOMA LAPONGEZWA KATIKA KUKABILIANA NA WAHAMIAJI HARAMU

    June 23, 2025
  • MRADI WA BARABARA MWANDIGA KAGUNGA AWAMU YA KWANZA WAFIKIA 95%

    June 21, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA WAANZA KAMBI YA MATIBABU KIGOMA

    June 16, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa