• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

Watu 40,000 kupata chanjo ya UVIKO 19 Mkoanj Kigoma

Posted on: August 3rd, 2021

Watu 40,000 kupata chanjo ya UVIKO 19 Mkoani Kigoma

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amezindua  rasmi zoezi la utoaji wa chanjo ya UVIKO-19 leo tarehe 03 Agosti 2021 katika kituo cha kutolea chanjo kilichopo katika Hospitali ya Mkoa ya Rufaa ya Maweni iliyopo katika manispaa ya Kigoma Ujiji.

Akizindua zoaezi la utoaji chanjo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye amesema katika  awamu ya kwanza chanjo inatarajiwa kutolewa kwa watu 1,708 katika vituo 24 vilivyopo katika almshauri za Mkoa wa Kigoma ambapo wananchi waliotayari kuchanjwa watajisajili katika mfumo wa Taifa wa Chanjo ama katika vituo vilivyo chaguliwa katika Halmashauri husika na watapatiwa cheti baada ya kuchanjwa.

Uzinduzi wa chanjo hii katika Mkoa wetu wa Kigoma, unatoa fursa kwa Wananchi ambao wako tayari kuchanjwa kupunguza kasi ya maambukizi ya ugonjwa pamoja na kupunguza hatari ya kupata ugonjwa na madhara makubwa endapo mtu atapata maambukizi. Amesema Andengenye.

Amesema zoezi la kuchanja litafuata Mwongozo wa Chanjo wa Taifa dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO-19, Shirika la Afya Duniani (WHO), ambapo amebainisha kuwa chanjo hizi kwa sasa zinatolewa kwa kufuata vipaumbele vya makundi yenye uhitaji mkubwa ambayo Watumishi wa sekta ya Afya, watu wazima wenye umri wa miaka 50 na kuendelea na watu wenye magonjwa sugu, amesisitiza kuwa uchanjaji kwa makundi yote ni wa hiari au huru kwa kila mwananchi

Andengenye ametoa onyo  kwa taasisi itakayotoza gharama ya aina yoyote katika utoaji wa chanjo hiyo ambayo ni bure kwa kila mhitaji alisema ā€œnaelekeza  kwa huu mgao wa COVAX FACILITY ni marufuku Hospitali yoyote (ya umma au binafsi) kulipisha Wananchi gharama yoyote katika zoezi hili la chanjo na lifanyike kwa uadilifu na kwa haki kwa walengwa wa sasa

Andengenye ameipongeza Serikali ya awamu ya Sita chini ya Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kufanikisha upatikanaji wa chanjo hii hapa nchini pia ameendelea kuwasisitiza Wananchi kuendelea kujikinga na UVIKO-19 kwa kunawa mikono, kuvaa barakoa, kukaa umbali za mita moja au zaidi, kuepuka misongamano na kufanya mazoezi.

Amewataka Wanahabari, Wananchi, Viongozi wa Jamii, Viongozi wa madhehebu ya Kidini na wengineo kuhakikisha wanapeleka ujumbe kwa jamii kuhusu huduma za chanjo, kuwaelimisha na kuwaelekeza Wanachi kwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya ili wapate chanjo.

Kwani Jamii ya Kigoma ikiwa imekingwa itapunguza milipuko ya mara kwa mara ambayo husababisha magonjwa na vifo.  Vilevile jamii ikichanjwa itadumisha kiwango cha juu cha chanjo na hivyo kuboresha uchumi na maisha kwa ujumla alisema Mkuu wa Mkoa.

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeanza kufanya usambazaji wa chanjo za UVIKO-19 katika Mikoa kumi iliyoripotiwa kuwa na maambukizi mengi ya Ugonjwa wa UVIKO 19 hapa nchini ukiwemo Mkoa wa Kigoma ambapo chanjo aina ya Janssen kutoka     Kampuni ya Johnson & Johnson ya nchini Marekani ndiyo inayotolewa..




Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa