• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WATOTO 505,840 KUPATIWA KINGATIBA KIGOMA

Posted on: November 22nd, 2023

KATIBU TAWALA MKOA WA KIGOMA ALBERT MSOVELA AKITOA TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI (HAWAPO PICHANI) KUHUSU ZOEZI LA UTOAJI WA KINGATIBA  KWA AJILI YA KUDHIBITI   MAGONJWA YA MINYOO YA TUMBO NA KICHOCHO MKOANI KIGOMA.

MRATIBU WA MAGONJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE MKOA WA KIGOMA INNOCENT MSILIKALE AKISHIRIKI KATIKA  MKUTANO WA KATIBU TAWALA NA WAANDISHI WA HABARI ULIOLENGA KUTOA TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UTEKELEZAJI WA ZOEZI LA UTOAJI WA KINGATIBA  MKOANI KIGOMA. 

Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI inaendesha zoezi la umezeshaji vidonge vya Kingatiba kwa ajili ya kudhibiti magonjwa ya Minyoo ya tumbo na Kichocho kwa watoto kuanzia umri wa miaka mitano hadi 14 katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na Magharibi ikiwemo mkoa wa Kigoma.

Akitoa Taarifa kwa Umma kuhusu uendeshaji wa zoezi hilo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Albert Msovela amesema mkoa umepokea jumla ya vidonge 793,000 aina ya Plaziquantel na 548,200 aina ya Albendazole  kwa lengo la kuchanja watoto 505,840 walioko ndani nan je wa utaratibu wa shule.

Amesema Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele, imedhamiria kutekeleza mpango huo ili kuhakikisha watanzania wanakuwa na Afya Bora kwa kuwakinga dhidi ya magonjwa yanayoweza kuzuilika.

Amesisitiza kuwa, ili malengo ya serikali yaweze kufikiwa, Jamii inapaswa kutoa ushirikiano kwa wataalam wa Afya katika kuwatambua walengwa na kuhakikisha wanafikiwa kisha kupatiwa huduma.

‘’Nitoe wito kwa wadau mbalimbali wa Afya na Jamii kwa ujumla kuhakikisha tunashirikiana na srikali katika utekelezaji wa zoezi hili ili walengwa wote waweze kufikiwa, aidha Jamii ikumbuke wajibu wake wa kuhakikisha watoto wote wanapatiwa chanjo kuendana na miongozo ya wizara ya Afya’’ amesisitiza Msovela.

Akitoa taarifa ya Maendeleo ya utekelezaji wa zoezi hilo Mratibu wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele mkoa wa Kigoma, Innocent Msilikale amesema utekelezaji wa zoezi hilo umekuwa ukikabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo uelewa duni wa wakazi kuhusu umuhimu wa zoezi hilo pamoja na hofu itokanayo na uwepo wa maudhi madogo madogo yatokanayo na matumizi ya dawa hizo.

Aidha Msilikale amesema katika kukabiliana na changamoto hizo, elimu kuhusu umuhimu wa kingatiba hizo inaendelea kutolewa kwa wazazi, walimu na jamii kwa ujumla sambamba na kuhamasisha ulaji shuleni wakati wa utoaji wa dawa hizo

Zoezi la ugawaji kingatiba ya magonjwa ya minyoo na kichocho limeanza kutekelezwa kuanzia tarehe 13 hadi 24, Novemba 2023 likihusisha Halmashauri nane za mkoa wa Kigoma.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa