• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WATAALAM TIMU YA UTEKELEZAJI MRADI WA BOOST WAJENGEWA UWEZO

Posted on: December 22nd, 2022


Wataalam wa Timu za Utekelezaji wa Mradi wa kuboresha Elimu ya Awali na Msingi ‘’BOOST’’ Kanda ya Magharibi wameshiriki mafunzo elekezi kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa utekelezaji wa Mradi huo, yaliyofanyika Leo Desemba katika Chuo cha Ualimu Kasulu Mkoani hapa.

Awali akifungua Mafunzo hayo, Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Kigoma Bi. Paulina Ndigeza amewasisitiza washiriki kuwa, mara baada ya mafunzo hayo wakatekeleze wajibu wao kwa uthabiti ili kupata matokeo chanya katika Sekta ya Elimu kama ambavyo Serikali inavyotarajia.

‘‘Tutumie nafasi hii kujifunza kwa bidii na tuhakikishe tunaelewa dhamira ya Mradi huu kwa kuwa malengo ya Serikali na Wahisani ni kuhakikisha tunafanya maboresho makubwa katika mfumo wa Elimu nchini ikiwemo kuongeza udahili wa Elimu awali pamoja na kujenga Mazingira rafiki ya ujifunzaji na ufundishaji’’ amesema Ndigeza.

Aidha, amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza kiasi kikubwa cha Fedha katika kuimarisha Miundombinu ya Elimu pamoja na kuchukua hatua za kuwezesha utekelezaji wa kazi  mbalimbali za kielimu nchini.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo Bi. Joyce  Mushi kutoka OR-TAMISEMI, Amesema Mradi huo wa BOOST wenye thamani ya Shilingi Tril. 1.15 ambazo ni ufadhili kutoka Benki ya Dunia,  umelenga kuzifikia Shule 6000 na kuwafikia zaidi ya watoto Milioni 12 nchini.

Amewasisitza wanamafunzo kutanguliza uzalendo ili kufikia malengo jambo litakalotoa fursa ya kuendelea kuaminiwa na kupata mikopo zaidi ili kubotresha na kuimarisha Sekta ya Elimu.

‘‘Kama ambavyo tunaendelea kuwaelekeza, hakikisheni mnaenda kufanya kazi kuendana na Miongozo na Mafundisho tunayowapatia, hii itatoa fursa ya kuendelea kupata misaada zaidi ambayo itatoa nafasi ya kuwagusa watu wengine kwani mahitaji yetu katika kuiimarisha sekta ya Taaluma ni makubwa sana’’

Mafunzo hayo ya Siku mbili yanaratibiwa na kutekelezwa kwa ushirikiano wa Wizara ya OR-TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Fedha ambapo  washiriki wanajengewa uwezo katika Afua za Uboreshaji wa Miundombinu, Uwekaji Mazingira Salama ya Ufundishaji na Ujifunzaji, kuongeza  udahili wa Wanafunzi wa  Elimu awali, Uboreshaji mazingira ya kielimu, utoaji mafunzo endelevu kwa walimu kazini, kuwezesha upatikanaji wa Rasilimali za utoaji Huduma katika Halmashauri.

Timu za utekelezaji wa Mafunzo hayo, zinaundwa na wakuu wa Idara na Vitengo vya Elimu Msingi, Manunuzi, Maendeleo ya Jamii, Uthibiti Ubora wa Elimu, Walimu ngazi ya Shule za Msingi, Wahandisi, Maafisa Habari pamoja na Mratibu wa Mradi ngazi ya Mkoa.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa