• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WANUFAIKA TASAF WATAKIWA KUJIUNGA NA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI

Posted on: June 12th, 2024

Wanufaika wa Mpango wa kunusuru Kaya Masikini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) mkoani Kigoma wametakiwa kujiunga na vikundi vya wajasiriamali ili kupata fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwemo mikopo yenye riba nafuu kutoka kwenye taasisi rasmi zinazotambulika  kiserikali.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma alipozungumza na wanufaika wa mpango huo mara baada ya kufunga Kikao kazi cha Viongozi wa Mkoa na Wilaya kilichofanyika mjini Kasulu kwa lengo la kufanya tathmini ya utekelezaji wa mradi kwa kipindi cha 2023/2024 na kuwasisitiza wanufaika umuhimu wa kutumia fedha wanazopata kuendana na malengo ya serikali ikiwemo kufanya shughuli za uzalishaji mali.

Amesema suala la kuitwa masikini sio sifa hivyo inapopatikana fursa ya kujikwamua kiuchumi na kujitoa katika kundi hilo, wananchi wanapaswa kuchangamkia nafasi hizo ili wwaweze kumudu kuendesha maisha yao bila utegemezi wa misaada kutoka kwa wahisani mbalimbali pamoja na Serikali.

''Tumepata shuhuda mbalimbali pamoja na kujionea namna ambavyo mpango huu umefanikiwa kubadili maisha ya wanufaika ikiwemo kununua mashamba, kujenga makazi bora, kuongeza tija kwenye kilimo, kusomesha, kuanzisha na kuimarisha biashara pamoja na kutatua changamoto za kifamilia ikiwemo uhakikika wa upatikanaji wa chakula na matibabu'' amesema Andengenye.

Aidha Andengenye amewasisitiza wanufaika kutumia fedha wananyoipata kuhakikisha watoto wao  wanahudhuria shuleni, wanapata matibabu kwa wakati, wanapata lishe bora pamoja na kuwakinga na maradhi ili waweze kuwa timamu kimwili na kiakili.

David Mzirai ambaye ni Afisa Ufuatiliaji Mradi wa TASAF kwa wilaya ya Kigoma amesema kumekuwa na changamoto ya baadhi ya wanufaika kutofuzu pamoja na kufikia malengo au sifa zinazostahili, jambo linalonyima fursa kwa wahitaji wengine kufikiwa na huduma hiyo.

Aidha amesisitiza kuimarishwa kwa mikakati itakayosaidia kuondoa wimbi la wanufaika wasio na sifa ili kutoa fursa kwa wahitaji wenye sifa kupata huduma hiyo kama ilivyokusudiwa na serikali

Mzirai ameahidi kuendelea kushirikiana na uongozi unaosimamia mradi ili kudhibiti watu wasio na sifa kuendelea kunufaika sambamba na kuwahamasisha wenye sifa kuhudhuria kwenye warssha za kijamii ili kuwajengea uwezo kimatumizi.

Upande wake Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma CPA Johnson Gamba ameshauri Serikali kupitia waratibu wa Mpango huo kuweka muda rasmi wa ukomo kwa wanufaika ili kutoa fursa kwa watanzania wengine wenye uhitaji kufikiwa na huduma hiyo.

Wakitoa ushuhuda wa manufaa waliyoyapata kupitia mradi huo, Cesilia Richard amesema kupitia mradi huo, ameweza kujenga nyumba ya vyumba viwili, kusomesha watoto pamoja na kuimarisha biashara anayoifanya.

Amesema kupitia mradi wa TASAF amefanikiwa kupata mtaji unaomfanya aweze kuendesha maisha yake na familia kwa ujumla na kumpunguzia adha ya kutegemea ndugu na jamaa.

Kupitia ushuhuda huo walioutoa mbele ya Mkuu wa Mkoa, Bi Leonia Hwaga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia kwa kuufanya mradi huo kuwa endelevu ambapo amefanikiwa kuanzisha ufugaji, amenunua mashamba mawili pamoja na kusomesha watoto wawili.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa