• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WANUFAIKA TASAF KASULU WAKUMBUSHWA KUTUMIA FEDHA WANAZOPATA KUENDANA NA MALENGO YA SERIKALI

Posted on: May 30th, 2024

WANUFAIKA WA MRADI WA TASAF MTAA WA MWINYI MJINI KASULU WAKIKABIDHI ZAWADI YA MBUZI KWA MKUU WA MKOA WA KIGOMA THOBIAS ANDENGENYE ALIPOFANYA ZIARA WILAYANI HUMO KWA LENGO LA KUKAGUA MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MRADI HUO.

Wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF) mkoani Kigoma wametakiwa kutumia fedha wanazozipata  kutokana na mradi huo kwa kuzingatia malengo yaliyokusudiwa ili waweze kuongeza kipato na kuboresha maisha yao.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wakazi wa Wilaya za Buhigwe, Kasulu na Uvinza, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema njia pekee ya kunufaika na fedha hizo ni kuunganisha nguvu miongoni mwao na kuanzisha miradi midogo midogo ili waweze kuzalisha kupitia kiasi cha fedha wanachopokea na kutimiza malengo wanayojiwekea.

WANUFAIKA WA MRADI WA TASAF MTAA WA MWINYI MJINI KASULU WAKIFUATILIA UTOAJI TAARIFA YA MRADI WA SHAMBA LAO LA MITI KWA MKUU WA MKOA WA KIGOMA.

Andengenye amewakumbusha wanufaika wa mradi huo kujikita katika shughuli za uzalishaji ambazo hazitohitaji gharama kubwa kiuendeshaji na kuwawezesha kupata kipato kitakachokidhi mahitaji yao.

Amesema lengo la Serikali kupitia mradi huo ni kuhakikisha watanzania wenye kipato kidogo wanaweza kumudu gharama za maisha ikiwemo kupata matibabu, chakula, makazi, mitaji midogo ya Biashara sambamba na kuwezesha gharama za manunuzi ya mahitaji ya shule kwa wanafunzi kutoka kaya hizo.

ENEO LA SHAMBA LA KIKUNDI CHA WANUFAIKA WA TASAF KATA YA MWINYI LENYE MITI 900 AINA YA PINUS. SHAMBA HILI AWALI LILIKUWA ENEO LA KUHIFADHIA TAKA LAKINI KWA SASA LIMEGEUKA NEEMA KWA WAKAZI HAO KWANI SAMBAMBA NA UWEPO WA MITI HUPANDA MAHARAGE NA MAHINDI KISHA KUGAWANA KWA AJILI YA CHAKULA.

Akiwasilisha   Taarifa ya Mradi wa Shamba la miti unaotekelezwa na walengwa wa mpango wa TASAF Mtaa wa Mwinyi wilayani Kasulu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Vumilia Simbeye amesema katika kipindi cha mwaka wa Fedha 2022/2023 jumla ya miradi 106 ilitambuliwa ikiwa imegawanyika katika sekta za Mazingira pamoja na ujenzi wa Miundombinu.

Ameendelea kusema mpango huo umeendelea kuwa mkombozi mkubwa kwa wakazi wengi wanaotoka katika kaya masikini na kuwafanya kumudu gharama ndogondogo za maisha sambamba na kusomesha watoto.

Abdallah Ibrahim mkazi wa Kasulu mji, ambaye pia ni mnufaika wa mpango huo amesema  kupitia fedha wanazopata wao kama wanufaika katika kata ya Mwinyi, wameanzisha kilimo cha miti na mazao ya chakula katika eneo lililokuwa likitumika kihifadhia taka mjini hapo.

Leticia Kagabo ambaye pia ni mnufaika wa TASAF amesema fedha aliyoipata kupitia mpango huo imemuwezesha kusomesha watoto wawili pamoja na kupata fedha ya pango, huku akisisitiza wanufaika wengine kutotumia fedha hizo kwa kufanya starehe au mambo mengine yaliyo nje ya malengo ya serikali.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa