• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WANUFAIKA MAZAO YA UVUVI WAUNGA MKONO UPUMZISHWAJI ZIWA TANGANYIKA

Posted on: May 10th, 2024

#

Baadhi ya Boti za kisasa zilizokabidhiwa kwa wavuvi mkoani Kigoma na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega.


Wananchi wanaojishughulisha na Uvuvi katika Ziwa Tanganyika wameonesha kuridhishwa na hatua ya Seikali kusitisha kwa muda wa miezi mitatu shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika ili kulipa nafasi ya kuongeza kiwango chake cha uzalishaji wa Samaki.

Hatua hiyo  muhimu imefikiwa wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vizimba vya kufugia Samaki, boti za kisasa za uvuvi na za doria pamoja na zoezi la utoaji wa Elimu  kwa wavuvi kuhusu umuhimu wa upumzishaji wa shughuli za uvuvi kwa muda katika ziwa Tanganyika, iliyofanyika katika Mwalo wa Katonga katika manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani hapa.

Akikabidhi vitendea kazi hivyo kwa walengwa wanaofanya Shughuli za Uvuvi katika ziwa hilo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu ametoa zana hizo  ili kuwezesha wananchi kufanya ufugaji wa kisasa ikiwa ni njia mbadala ya kujipatia kipato  katika kipindi ambacho ziwa hilo litakuwa limepumzishwa.

Aidha Waziri Ulega amewataka wanufaika wa vitendea kazi hivyo kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa  huku akiwataka maafisa uvuvi katika ukanda wa ziwa Tanganyika kuongeza kasi ya utoaji wa Elimu  kwa wavuvi na wakazi ili waweze kushiriki katika kufanukisha zoezi hilo.

Mara baada ya kushuhudia ugawaji huo wa vitendea kazi,  Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Kirumbe Ng’enda amesema upumzishwaji wa Ziwa hilo umezingatia muda ambao ziwa hupunguza uzalishaji wake.

Amesema kuwa, kwa muda mrefu wavuvi wamekuwa wakitumia gharama kubwa kubwa bila kupata faida kutokana na kiwango cha upatikanaji wa samaki katika ziwa hilo kup[ungua na kusababisha kupata  hasara.

Upande wake mbunge wa Kigoma Kusini Nashon Bidyanguze amesema ukosefu wa Elimu ya umuhimu wa upumzishaji wa ziwa hilo ulichangia kwa kiasi kikubwa kususa sua kwa zoezi hilo katika kipindi cha nyuma, lakini kwa sasa wavuvi na wakazi kwa ujumla wanaelimu ya kutosha juu ya umuhimu wa kufungwa kwa ziwa Tanganyika.

Katika hafla hiyo, Waziri Ulega amekabidhi vizimba 29 kwa vikundi sita na watu binafsi  16 sambamba na boti kwa ajili ya uvuvi na doria  katika mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa.

Hafla hiyo imehuduriwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye,  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kigoma, wabunge wa Majimbo ya Kigoma Mjini na Kigoma Kusini, Kamati ya Usalama Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, watendaji wa Serikali sambamba na wadau mbalimbali wa shughuli za uvuvi mkoani hapa.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa