• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WANAUME WAASWA KUJITOKEZA KUPIMA VVU

Posted on: December 1st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi  la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye amewaasa wanaume mkoani hapa kujitokeza kwa wingi na kuwa mstari wa mbele katika  kuziendea huduma za upimaji wa  Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ili kujua hali zao kiafya kwa lengo la kupunguza maambukizi na athari kwa waliokwisha ambukizwa ugonjwa huo.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo, alipozungumza na wananchi wa mkoa wa Kigoma waliojitokeza kushiriki maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika Halmashauri ya wilaya ya Kakonko.

Amesema wanaume wengi wameendelea kuishi kwa hofu huku wakiogopa kuujua ukweli kuhusu hali zao kiafya jambo ambalo ni hatari kwa waliokwisha pata maambukizi kutokana na athari zinazoweza kujitokeza kwa sababu ya  kuchelewa kuanza kutumia dawa za kufubaza makali ya maradhi hayo.

‘‘Nyote mnatakiwa kuwa mstari wa mbele kwa kuongozana na wenzi wenu  wa ndoa kupima hali zenu kiafya na iwapo nyote au mmoja wenu atabainika kuwa na maambukizi  aanze kupata matibabu mapema na kujihakikishia Afya njema na maisha yenye furaha’’ amesema Andengenye.

Ameongeza kuwa, kati ya wanaoishi na VVU wenye Umri wa Miaka 15 hadi 64, wanaoendelea kutumia dawa na Asilimia 98.5 wanaonyesha kufanikiwa kufubaza maradhi hayo ambapo wanawake ni Asilimia 98.5 na Wanaume ni Asilimia 98.5.

Aidha, Mkuu wa Mkoa Amesisitiza kuzingatia Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka 2022, kwani ujumbe wake unalenga kuimarisha hali ya usawa na kuondoa vikwazo katika  Nyanja zote zinazotekeleza Afua mbalimbali za kupambana na kudhibiti Maambukizi ya VVU na Ukimwi pamoja na Jamii.

Awali akitoa taarifa ya Mkoa kuhusu maendeleo ya Utekelezaji wa Afua mbalimbali za UKIMWI, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Jesca Lebba, amesema Serikali inaendelea kuboresha na kuimarisha miundombinu mbalimbali ya Afya hasa katika upimaji wa Virusi vya Ukimwi.

‘’Hatua mbalimbali zimeendelea kuchukuliwa katika kuhamasisha na kuhakikisha wananchi wanatambua umuhimu wa kujua Afya zao na wenye maambukizi wanakuwa na utayari wa kutumia dawa za kufubaza makali ya virusi vya Ukimwi, jambo ambalo tunaendelea kulitekeleza kwa mafanikio makubwa’’amesema Dkt. Lebba.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kushiriki Maadhimisho hayo, wamekiri kuwepo kwa tatizo la muitikio hasi kwa wanaume wengi katika kuziendea huduma za upimaji wa virusi vya Ukimwi hususani katika Maeneo ya vijijini.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa