• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WANANCHI WA MKOA KIGOMA WAMEJITOKEZA KATIKA KUPATA MATIBABU KUTOKA KWA MADAKTARI BINGWA

Posted on: May 22nd, 2017

Mamia ya wananchi wa Mkoa Kigoma wamejitokeza katika kupata matibabu kutoka kwa madaktari bingwa ,  mpango unaoratibiwa na Mfuko wa Taifa wa bima ya afya nchini (NHIF).

Matibabu hayo yanayotolewa katika hopsitali ya Mkoa Kigoma Maweni yanahusisha magonjwa ya kina mama ,magonjwa ya moyo,magonjwa ya watoto ambayo madaktari bingwa wake watafanya kazi hiyo moja kwa moja huku magonjwa mengine ambayo hayana madaktari bingwa yatatolewa ushauri wa hatua za kuchukua.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya mfuko huo, Anne Semamba  Makinda amesema kuwa hakuna mtanzania atakayekufa kwa sababu ya kukosa pesa za matibabu kutokana na serikali ya awamu ya tano kuweka mfumo mzuri unaohakikisha wananchi wote wanapata matibabu kwa gharama nafuu.

Mkuu wa wilaya Kigoma Samson Anga (Wa pili kulia) na Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya mfuko wa Taifa wa bima ya afya (Anne Makinda) wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa utoaji huduma kupitia mpango wa madaktari bingwa wanaotembea utakaofanyika mkoani Kigoma Kwa wiki moja.


Mama Anne alisema kuwa kwa sasa wananchi wote wataweza kujiunga na huduma za matibabu za mfuko huo kupitia makundi mbalimbali yalipo kwenye jamii na mitaa na wananchi watapata huduma za matibabu nchi nzima bila kubagua hospitali.

Aliongeza kuwa pamoja na hilo mfuko huo unatambua kuwepo kwa changamoto za uhaba wa madawa, vitendea kazi, uchache wa majengo na vifaa vingine vya kutolea tiba na kwamba mfuko huo umzingatia changamoto hiyo na kwa sasa mfuko unatoa mikopo kwa vituo vya afya, zahanati na hospitali ili kuwezesha huduma bora kupatikana wakati wote.

Akizungumzia utoaji huduma kwa wagonjwa alisema kuwa mfuko unapokea malalamiko ya wananchi kuhusiana na lugha mbaya na za kuudhi zinazotolewa na watoa huduma na kwamba ikithibitika kwamba yupo mtoa huduma ametoa lugha mbaya kwa wagonjwa watachukulia hatua za kinidhamu kwa mujibu wa taratibu za kiutumishi.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bw. Bernad Konga alisema kuwa mfuko unatambua changamoto iliyopo ya uhaba wa madaktari bingwa uliopo nchini na ndiyo maana mfuko umeanzisha mpango wa huduma za madaktari bingwa wanaotembea ili kuweza kuwafikia wananchi.

Pamoja na kutoa huduma kwa wananchi Bw. Konga alisema kuwa mpango huo pia unalenga kutoa mafunzo kwa watoa huduma waliopo kwenye vituo ambavyo mpango huo unatekelezwa ili waweze kuendeleza huduma husika baada ya madaktari bingwa hao kuondoka.

Alisema kuwa tangu kuanza kwa mpango huo jumla ya wananchi 13,000 wamefikiwa na kati yao zaidi ya 600 wamepatiwa huduma za upasuaji wa magonjwa mbalimbali na hivyo kufanikisha mpango wa kuwafikia wananchi kwa karibu.

Akisoma hotuba kabla ya kuzindua mpango huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Kigoma, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bw. Samson Anga alisema kuwa kumekuwa na uhitaji wa madaktari bingwa Mkoani humo ikizingatiwa kuwa kwa sasa mkoa unao madaktari bingwa wawili tu jambo ambalo linafanya wananchi kutumia muda na gharama kubwa kutafuta huduma hizo nje ya mkoa.

Katika hotuba hiyo Mkuu wa wilaya Kigoma,Samosn Anga alisema kuwa mpango huo ni wa maana sana kwani utawasaidia wananchi wa mkoa huo kupunguza makali ya upatikanaji wa huduma hiyo kwa wakati huu na kwamba serikali ya mkoa itatoa ushirikiano wa hali na mali kuhakikisha utekelezaji wa mpango huo unakuwa wa mafanikio.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa