• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAKIMBIZI KUTOKA BURUNDI MKOANI KIGOMA WAANZA KUREJEA KWAO

Posted on: September 7th, 2017

Kundi la kwanza la wakimbizi 301 wa Burundi waliokuwa wakihifadhiwa Nchini Tanzania kwenye kambi ya Nduta wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma limeanza kurejea nchini Burundi huku viongozi wa nchi hizo mbili wakisema kuwa ni heshima kubwa kwa wakimbizi hao kurudi nchini kwao sasa.

Mkuu Wa Mkoa Kigoma, Brigedia Jenerali Mstaafu Emanuel Maganga aliongoza uzinduzi rasmi wa zoezi hili huku akisema kuwa takribani wakimbizi 12,000 wanatarajia kurudishwa kwao hadi kufikia Desemba 31 mwaka huu ikiwa ni awamu ya kwanza ya utekelezaji wa zoezi hilo.

Alisema kuwa kwa sasa wakimbizi hao watarejeshwa kwa hiari kulingana na mikataba ya kimataifa ya kuhifadhi na kurejeshea kwao wakimbizi ambayo Tanzania imeridhia.

Awali Mratibu wa Idara ya Wakimbizi kanda ya Magharibi Nchini Tanzania, Bw. Tonny Laizer alisema kuwa kwa sasa wakimbizi watakaorejeshwa ni wale watakaojitokeza na kuandikishwa kwa hiari kurudi kwao.

Laizer aliongeza kuwa awamu ya pili ya zoezi hilo litafanyika kwa uhamasishaji kwa viongozi Wa serikali ya Burundi kutembelea makambi kuzungumza na wakimbizi hao sambamba na baadhi ya wakimbizi kupelekwa kutembelea Burundi kuona hali ya amani na usalama iliyopo nchini humo ili kuwashawishi wakimbizi wenzao kujiandikisha kurudi nchini mwao kwa hiari.

Kwa upande wake Makamu Waziri wa mambo ya ndani wa Burundi, Terence Ntahiraja akinukuu maneno aliyotoa Raisi Pierre Nkurunzinza wa Burundi Julai 19 mwaka huu Ngara Mkoani Kagera nchini Tanzania kuwa Burundi ina amani ya uhakika na watu hao hawana sababu ya kuishi uhamishoni kama wakimbizi.

Ntahiraja alisema kuwa baadhi ya wakimbisi ambao hawako tayari kurudi kwa madai ya hali ya amani haijatengemaa nchini humo wanayo fursa kwenda kutembea kuona hali halisi na kuamua huku akionya baadhi ya wakimbizi wanaohamasisha wakimbizi wenzao wasirejee kwa kigezo cha hali mbaya ya usalama.

Kuhusiana na hali ya kiuchumi ya wakimbizi hao Waziri huyo wa mambo ya ndani alisema kuwa serikali ya Burundi inaweka mazingira mazuri kwa wakimbizi hao kurejea kwenye maisha yao kawaida kwa kuandaa mipango ambayo itakuwa na msaada wa kiuchumi kwa wakimbizi hao.

Dafroza Mugabekazi na Mwamvita Emanuel ni miongoni mwa wakimbizi walioanza safari ya kurudi Burundi ambapo wamesema kuwa wameamua kurudi Burundi kujenga maisha yao baada ya amani kurudi huku wakieleza kuchoshwa na maisha ya ukimbizi.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa