• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAKAZI MKOANI KIGOMA WATAKIWA KUENDELEZA UJENZI RAFIKI KWA MAZINGIRA

Posted on: September 13th, 2022

Wakazi Mkoani  Kigoma wametakiwa kuendeleza shughuli za ujenzi huku wakichukua tahadhari dhidi ya uharibifu wa Mazingira  na kuifanya dunia kuwa sehemu salama kwa maisha ya sasa na  kwa vizazi vijavyo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mhe. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Selemani Jafo alipofika mkoani hapa kwa lengo la kutoa maelekezo kuhusu zuio  la Serikali la kutokuendeleza makazi katika Kata ya Sanganigwa iliyopo manispaa ya Mji Kigoma-Ujiji ambapo aliidhinisha kuendelea kwa shughuli hizo  kufuatia Serikali kujiridhisha kuhusu kutowepo kwa athari za kimazingira katika eneo hilo.

Alisema maeneo yote ambayo wananchi wanataka kuendeleza makazi na shughuli nyingine za maendeleo zinazohusisha ujenzi, wahakikishe wanapata ushauri kutoka kwa wataalam wa ujenzi na wale wa mazingira ili kuepusha athari zitokananzo na shughuli hizo.

‘‘Baadhi ya Wataalam ama kwa uzembe au kutokujua wamekuwa wakiruhusu wananchi kujenga katika vyanzo vya Maji, maeneo ya uhifadhi na hata maeneo hatarishi kwa usalama, bila kutoa maelekezo yanayoambatana na ushauri pamoja na tahadhari.’’ Alisema Jafo.

Aliwaagiza wataalam wa Mazingira kutoa ushauri na maelekezo kwa Serikali na pamoja na wananchi pale wanapoona kunampango wa uanzishwaji wa shughuli za kibinaadam katika eneo ambalo uharibifu wa kimazingira unaweza kutokea  ili kuepusha usumbufu na hasara zinazoweza kuwakuta wananchi wa eneo hilo.

Aidha Waziri Jafo alielekeza Ujenzi unaofanyika maeneo yote nchini  uzingatie utaratibu wa uvunaji  wa Maji ya Mvua kwa lengo la matumizi  ili kupunguza gharama na matumizi makubwa ya maji katika makazi.

‘’Naelekeza maeneo yote ya Majiji, Miji, Manispaa na wilaya ujenzi wa makazi uambatane na utaratibu maalum wa uvunaji  Maji ya mvua kuliko kuyaacha yapotee bure huku tunauhitaji mkubwa wa Maji hayo kwa matumizi yetu’’alisema Waziri Jafo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa