• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAKAZI KALILANI WALIPWA FIDIA KUPISHA ENEO LA HIFADHI MSITU WA MAHALE

Posted on: February 25th, 2025


Serikali kupitia imelipa fidia kiasi cha Shilingi Bilioni 1.68 kwa wakazi wanaoishi eneo lililokuwa  Kitongoji cha Kabukuyungu na Mahasa katika Kijiji cha Kalilani Kata ya Buhingu Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma  kutokana na eneo hilo  kuwa chini ya umiliki wa Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Mahale.

Zoezi hilo limefanyika  ili kupisha uhifadhi wa Mazingira endelevu kwa ajili ya hifadhi ya wanyama jamii ya Sokwe ambapo kwa hatua ya awali  jumla ya  kaya 205 kati ya kaya 376 ambazo wakazi husika waliridhia kufanyiwa Tathmini ya mali zao zimelipwa huku uongozi wa Serikali ya Mkoa ukitoa Rai kwa kaya ambazo hazijafanyiwa tathimini kuchukua hatua ili  kuepusha hasara ikiwemo kupoteza makazi  yao baada ya Siku Sitini kuanzia Februari 25,2025 ambapo maeneo hayo yatarejeshwa rasmi kwenye umiliki wa Hifadhi hiyo.

Zoezi la ulipaji wa fidia, limeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye, ambapo ameitaka jamii kuendelea kulinda Mazingira na viumbehai ikiwemo wanyamapori katika maeneo ya hifadhi ili kudumisha urithi huo wa Asili  kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.

Amesema wakazi wanapaswa kutambua umuhimu wa kulinda rasilimali za nchi ikiwemo mnyama Sokwe, ambao wanazidi kuadimika nchini  kutokana uharibifu wa Mazingira huku akisisitiza ulinzi wa  hifadhi ya Mahale na maeneo mengine tengefu mkoani Kigoma kwa ajili ya kutunza Mazingira na kudumisha Sekta ya Utalii ambayo inamchango mkubwa katika pato la Taifa.

Afisa Mhifadhi Mkuu Kharidi Mgofi ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Hifadhi ya Milima ya Mahale, amepongeza Serikali kwa kuchukua hatua ya kuwabadilishia eneo la makazi wananchi hao kulikoenda sambamba na malipo ya fidia kwa kuwa kimsingi eneo hilo lilikuwa chini ya umiliki wa hifadhi tangu awali kabla ya kugeuzwa makazi. 

Aidha baadhi ya Wananchi, walionufaika na Mpango huo, wameupongeza uongozi Mkoa chini ya Utendaji kazi wa Serikali ya Awamu ya Sita kutekeleza zoezi hilo  kwa kuzingatia utu, jambo litakalowafanya kutohangaika watakapohamia katika makazi mapya.

Aidha, wakazi hao wamesema, hatua hiyo imeondoa sintofahamu  iliyokuwa ikiwakabili na kusababisha kusimama kwa shughuli za Maendeleo ambapo mara baada ya malipo hayo wameahidi kutekeleza agizo hilo kwa kuhamia maeneo waliyotengewa ili kuendelea na shughuli za uzalishaji mali.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa