• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAKALA WA MAJENGO MKOANI KIGOMA WAONYWA KUCHELEWESHA MIRADI

Posted on: January 4th, 2018


Wakala wa Majengo Tanzania TBA wameonywa kuwa na tabia za ucheleweshaji wa kumaliza miradi mbambali wanayopewa na Serikali jambo ambalo linakwamisha utoaji wa huduma katika miradi hiyo kama ilivyokusudiwa.

Serikali ilitoa fedha kwaajili ya ukarabati wa miundombinu kwa shule na vyuo vya zamani ambazo majengo yake na miundombinu ilikuwa imeshaakaa, kwa Mkoa wa Kigoma shule 16 ikiwemo Shule ya Sekondari ya Kigoam iliweza kupatiwa shilingi milioni 900, ambapo Mkandarasi Wakala wa Majengo Mkoani alipatiwa kazi hiyo.

Hata hivyo kumekuwa na kasi ndogo pamoja na utendaji usio wa kurishisha katika kufanya ukarabati wa miundombinu katika shule hiyo, kitendo ambacho kimefanya kuchelewa kukamilishwa kwa huduma muhimu kama vile vyoo, mabafu na mabweni.

Hadi kufikia muda wa wanafunzi kurudi kuanza muhula mwingine wa masomo mwaka 2018 bado wakala wa majengo Mkoani Kigoma walikuwa bado hawajakamilisha ukarabati wa miundo mbinu ikilinganishwa na fedha mabayo tayari imekwishakutolea awamu ya kwanza shilingi milioni 400.

Hali hii inamtia hasira si Waziri wa Elimu peke yake bali hata Mkuu wa MKoa wa Kigoma ambapo walipofanya ziara ya kukagua kazi zilizofanywa, ikaonekana ni mchezo wa kuigiza.

Akizungumza katika ziara ya kukagua ukarabati wa shule ya sekondari Kigoma Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce Ndalichako alimwambia Meneja Wakala wa Majengo Mkoani Kigoma kuacha ubabaishaji na kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano.

Inaonekana meneja hujui kazi yako, haiwezekani tangu mwezi Agosti 2017 mpaka leo hii hakuna kazi ya kuonekana uliyokwisha imaliza, wanafunzi wanasiku tatu wafungue bado vyoo havieleweki, unacheza na maisha ya binadamu, hili halikubaliki katika serikali ya awamu ya tano alisisitiza Prof. Ndalichako

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brig. Jen. Mstaafu Emmanuel Maganga ameshangazwa na kitendo cha wakala wa Majengo Mkoani Kigoma cha kushindwa kumaliza ukarabati wa  Shule ya sekondari ya Kigoma pamoja na kuwa Serikali imeshatoa fedha karibu nusu ya gharama kwaajili ya ukarabati tangu Agosti, 2017.

Kufuatia hatua hiyo amabayo inaashiria uzembe, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma aliamuru kuwekwa mahabusu Meneja wa Wakala Mkoani Kigoma Bw. Mgalla Mashaka kwa uzembe wa usimamizi na kushindwa kutoa maelezo sahihi ya nini kilichokwamisha kutomalizika kwa ukarabati wa shule hiyo.



Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa