• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAJUMBE MABARAZA YA ARDHI WATAKIWA KUTENDA HAKI

Posted on: May 17th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewataka wajumbe  wa mabaraza ya Ardhi na Nyumba mkoa wa Kigoma kuzingatia kanuni na maadili na miongozo ya utendaji kazi ili kutoa haki kwa wananchi wenye changamoto za migogoro ya ardhi mkoani Kigoma.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo mara baada ya kuwaapisha wajumbe wa mabaraza hayo kwa wilaya za Kakonko, Uvinza na Buhigwe na kuwataka kuepuka rushwa, upendeleo au kushiriki vitendo vyovyote vitakavyoashiria uvunjani wa sharia katika utoaji maamuzi dhidhi  ya walengwa.

‘’Wajumbe niwasisitize kiapo mlichoapa mkakitendee haki kwa kuepuka kutoa maamuzi na maoni kwa kuzingatia hisisa na mihemko bali kwa kuzingatia miongozo na ushahidi toshelevu unaotolewa ndani ya mabaraza’’

Amewasisitiza wajumbe hao kujenga tabia ya kusoma na kuelewa Sheria ndogo za mabaraza ili ziweze kuwa miongozo katika kufanya maamuzi hali itakayowaepusha na lawama zitakazotokana na kulalamikiwa kwa kufanya upendeleo.

Aidha kupitia kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma amemuelekeza Katibu Tawala Mkoa kuhakikisha wajumbe wa mabaraza hayo katika Halmashauri za Uvinza na Kakonko wanapatiwa Ofisi katika maeneo ya makao makuu ya Halmashauri na uwepo wa ofisi hizo utangazwe ili kuwarahisishia wananchi kutambua maeneo ya upatikanaji wa huduma hizo.

Nisisikie kuwa kuna wajumbe wa baraza la Ardhi na Nyumba wamekosa ofisi na hakikisha uwepo wa ofisi hizo unafahamika kwa wananchi ili wasiendelee kusumbuka kufuata huduma mbali na maeneo yao ya makazi.

Upande wake Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria Mkoa Diana Chove, amewataka wajumbe wa mabaraza hayo kujenga tabia ya kutafakari kwa kina kabla ya kutoa maamuzi kuhusiana na mashauri wanayoyaamua  ili kuharakisha upatikanaji wa suluhu.

Aidha amewakumbusha wajumbe hao kutoingilia majukumu yasoyowahusu bali wasimamie yale yaliyomo kwenye miongozo ya utendaji kazi wao.

Jumla ya wajumbe saba wa mabaraza hayo wameapa mbele ya mkuu wa mkoa wa Kigoma leo Mei 17,2024 kupitia hafla fupi iliyofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kuendana na Sheria ya Mahakama ya Ardhi Na. 2 ya Mwaka 2002 chini ya Kanuni Namba 36(1) na (2) GN na 174/2003.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa