• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAHIMIZWA KUENDELEZA UMOJA NA MSHIKAMANO ILI KUDUMISHA AMANI YA NCHI

Posted on: December 9th, 2022

Wananchi mkoani hapa wamehimizwa kuendelea kushirikiana katika kuimarisha Umoja na Mshikamano huku wakiwaenzi waasisi wa Taifa kwa kudumisha Amani iliyopo nchini ambayo ni chachu ya Maendeleo tuliyonayo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Michael Masala  kupitia Hotuba aliyoitoa alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka sitini na Moja ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu.

Amesema Msingi wa Amani, Umoja na Mshikamano tulionao ambao  uliwekwa na waasisi wa Taifa letu ni chachu kubwa ya maendeleo tuliyoyafikia kama Taifa   hivyo hatuna budi kuuendeleza na kuudumisha.

‘‘Tusikubali kuichezea Amani tuliyonayo na tunapaswa kuilinda kwa gharama  yoyote ili tusije kuupoteza Uhuru tulionao sasa, kwani bila kuwa huru hakuna uwepo wa maendeleo ya kweli’’Amesema Masala.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Albert Gabriel, amesema  nchi nyingi zinaonekana ziko Huru lakini hazina Amani ya kweli, hali inayosababisha kukosekana kwa utulivu wa wanchi katika kutekeleza majukumu yao ya kimaendeleao.

‘‘Tanzania imekuwa ni nchi  Huru na yenye Amani ya kweli tangu  ilipopajipatia Uhuru wake miaka 61 iliyopita na wananchi wanaendelea kutekeleza majukumu yao na kuishi kwa furaha, hivyo tuendelee kuitunza amani hiyo kwa mustakabali wa Maendeleo ya Taifa letu’’ amesisitiza Gabriel.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza na kushiriki katika Maadhimisho hayo, wamepongeza jitihada zinazoendelea kufanywa na viongozi wa Ngazi mbalimbali Serikali wakiongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu, kwa kuhakikisha amani iliyopo inadumu na kutoa fursa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo huku wananchi wakiendelea kuishi kwa furaha na upendo.

Aidha wakazi hao  wamesisitiza kuendelea kuyaenzi mawazo makuu ya Muasisi wa Taifa Mwal. Julias Kambarage Nyerere kwa kupambaana  na maadui Ujinga, Maradhi na Umasikini kwa kuhakikisha wanashiriki kwa dhati katika shughuli zote za maendeleo zinazotekelezwa kupitia miradi mbalimbali ya Serikali.

Viongozi mbalimbali wamehudhuria na kushiriki maadhimisho hayo wakiwemo wakuu Taasisi za Kiserikali, Binafsi na zile za kidini pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kigoma ambapo kauli mbiu ya Maadhimisho hayo kwa Mwaka 2022 ikiwa ni ‘’AMANI NA UMOJA NI NGUZO YA MAENDELEO YETU’’

PICHA: BAADHO YA WAKUU WA TAASISI ZA SERIKALI, TAASISI BINAFSI, VIONGOZI WA DINI, SIASA PAMOJA NA WANANCHI WALIOJITOKEZA KUSHIRIKI  KATIKA KILELE CHA MADHIMISHO YA  UHURU WA TANZANIA BARA YALIYOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA KASULU LEO TAREHE 9 DESEMBA 2022.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa