• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WADAU WA VIWANDA WAASWA KUTUMIA FALSAFA YA KAIZEN KUONGEZA TIJA NA UBORA KATIKA UZALISHAJI

Posted on: December 21st, 2022

Wadau wa Viwanda Mkoa wa Kigoma wametakiwa kutumia Falsafa ya KAIZEN ili kuboresha  hali ya utendaji kazi na kuimarisha uwezo katika uzalishaji wa bidhaa zitakazomudu ushindani katika Soko la Ndani na Nje ya Nchi.

Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Kigoma Sangu Deogratius, ametoa Rai hiyo alipokufungua Mafunzo yaliyoenda sambamba na uhamasishaji wa kutumia Falsafa ya KAIZEN katika Mkoa wa Kigoma, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Katibu Tawala Mkooani hapa.

Amesema ujenzi na Uchumi shindani unategemea ukuaji wa Sekta Imara ya viwanda na uwepo wa watendaji wenye ujuzi wakiwa na mtazamo unaozingatia uendelevu wa viwango bora na vyenye tija sambamba na uwezo wa kuihudumia Sekta hiyo.

‘‘Falsafa ya KAIZEN ndio Siri ya mafanikio ya nchi ya Japan katika uendeshaji wa viwanda na kujenga msingi imara wa kiuchumi unaolifanya Taifa hilo kuweza kuhimili ushindani wa Ubora wa Biashara katika Soko la Dunia’’ amesema.

Ameongeza kuwa,  Serikali ya Tanzania imepokea kwa mikono miwili ushirikiano na Serikali ya Japan kupitia JICA katika utoaji wa Mafunzo ya Falsafa hiyo ili kujenga hazina ya Rasilimali watu kwa ajili ya kujenga uchumi imara na shindani kimasoko kwa Maendeleo ya Taifa.

Aidha amewasisitiza wadau kuzingatia mafunzo hayo ili waweze kuwa mabalozi wazuri katika kutoa ushauri kwa wadau wengine ambao hawakupata fursa ya kushiriki kwa kueneza utamaduni mpya wa kufanya kazi viwandani kwa kufuata misingi ya falsafa ya KAIZEN.

Naye Deus John kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara ambaye pia ni Mkufunzi wa Falsafa ya KAIZEN, amesema Elimu hiyo imejikita katika kuwajengea uwezo wamiliki na wafanyakazi katika viwanda vikubwa, vya kati na vidogo ili kufanya uzalishaji wenye ubora utakaoendana na mahitaji halisi ya soko la ndani nan je.

Amesisitiza kuwa, Elimu ya KAIZEN inalenga kuvumbua mawazo  na maarifa yatakayosaidia kuboresha uzalishaji katika aina zote za viwanda, kuzalisha bidhaa zenye kiwango kinachokubalika katika Soko la Nje ili kuifanya nchi ya Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo Mwaka 2030.

‘‘Katika mikoa ambayo elimu hii imetolewa tayari wadau wameanza kupata matokeeo chanya kwa kuepuka hasara katika uzalishaji, kuzalisha bidhaa bora zenye kuhimili ushindani wa soko la ndani na lile la kimataifa’’ amesema.

‘‘Tunaendelea kutoa elimu hii katika Taasisi za Serikali pia ili wateja waweze kunufaika na utolewaji wa huduma bora katika ofisi za Serikali kwa kuwajengea uwezo watoa huduma ili watambue namna bora ya kutoa huduma kwa wateja wao’’ Amesema Deus.

Pia Emanuel Mgunda, Mthibiti Ubora wa uzalishaji katika Kiwanda cha Tanganyika Pure Drinking Water kilichopo mkoani hapa, amesema mafunzo waliyoyapata yataongeza thamani na tija katika uzalishaji viwandani katika Mkoa wa Kigoma na kuongeza thamani ya bidhaa hali iitakayosababisha kupanua wigo wa masoko.

‘‘Mkoa wetu umepakana na nchi jirani za Congo na Burundi, hivyo kutokana na uwezo tuliojengewa tumepata maarifa yatakayotusaidia kukabiliana na ushindani uliopo ili tuweze kumudu kuuza bidhaa zetu katika nchi hizo’’ amesema Emmanuel.

KAIZEN ni neno la kijapani lenye maana badilika kwa ubora au uzuri linalotumika kwenye biashara ambapo mpango huo unaotekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Serikali ya Japan inayotoa misaada ya maendeleo kwa nchi zinazoendelea  JICA, kwa lengo la kuimarisha Viwanda vya Uzalishaji kupitia uboreshaji wa Tija na Ubora.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa