• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WACHUNGAJI WAHIMIZWA KUSIMAMIA MAADILI YA KIIMANI

Posted on: May 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye akizungumza na waumini wa dhehebu la Anglican katika Kanisa la Mt. Andrea lililopo Kasulu Mjini aliposhiriki Ibada na kufungua Semina Maalum ya Ujasiriamali kwa wachungaji wa Dayosisi ya Western Tanganyika siku ya Tarehe 7 Mei, 2023.


Viongozi wa Madhehebu ya Dini mkoani Kigoma wamehimizwa kudumisha mafunzo na malezi bora ya kiimani kwa waumini wao ili kujenga Taifa lenye kizazi kitakachoenenda katika maadili mema na kujengeka katika misingi ya hofu na kumheshimu Mwenyezi Mungu.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobia Andengenye ametoa nasaha hizo aliposhiriki Ibada ya kusimikwa kwa Mchungaji Kanoni, Careb Zephania kuwa Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Wester Tanganyika Emmanuel Bwata pamoja na kufungua Semina  Maalum kwa wachungaji wa Dayosisi hiyo.

Amesema ongezeko la vitendo vya ukatili katika Jamii, uwepo wa chuki  na visasi baina ya ndugu, rushwa, dhuluma pamoja kuibuka kwa vitendo vya usagaji na ushoga  ni ishara ya ukosefu wa hofu ya Mwenyezi Mungu.

Ameendelea kufafanua kuwa, viongozi wa dini wanapaswa kutokukata tamaa na kuongeza juhudi katika kulibeba jukumu la kuuelimisha na kuuadilisha Umma ili uweze kuyatambua makusudi ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu na kuifanya Dunia kuwa Sehemu salama ya kuishi kwa kila Mtu.

Amesisitiza kuwa, Msingi wa Madhila ya kitabia na mienendo isiyo katika mfumo wa Tamaduni zetu tunayoishuhudia sasa isipokemewa na kudhibitiwa itaathiri kwa kiasi kikubwa kizazi chetu kijacho na kukifanya kuishi maisha yasiyo na utu, yaliyoja kufuru na machukizo mbele ya Mwenyezi Mungu na wanadamu wenyewe.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa amepokea ombi la Askofu  Mkuu wa Kanisa hilo Emmanuel Bwata, kusaidiwa kupata mbegu na miche ya chikichi kwa ajili ya kutimiza azma ya Kanisa kuanzisha mradi mkubwa wa Kilimo cha zao hilo.

Amefafanua kuwa, Serikali mkoani Kigoma inatambua umuhimu mkubwa wa kuinua uchumi wa wananchi kupitia zao hilo hivyo hatua madhubuti zitachukuliwa ili kuhakikisha uzalishaji wa miche na mbegu za chikichi unafanyika karibu na mazingira ya wahitaji ili kuwapunguzia adha.

Pia Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa Taasisi za kidini, vikundi mbalimbali vya waumini pamoja na watu binafsi kuanzisha vitalu vya zao la chikichi katika maeneo ya jirani na makazi yao na kuiarifu Serikali kupitia wataalam wa Kilimo ili waweze kupelekewa mbegu na kusaidiwa katika usimamizi wa uzalishaji wa Miche.

Ibada hiyo imefanyika  Sambamba na zoezi la uchangiaji wa fedha na vifaa vya ujenzi kwa ajili ya ukarabati mkubwa wa Kanisa la Mt. Andrea Dayosisi ya Tanganyika Magharibi lililopo Kasulu Mjini, ambapo Mkuu wa Mkoa amechangia Jumla ya Shilingi laki Tano na kuahidi kiasi kama hicho cha Fedha kwa ajili ya kuchangia vikundi vya Wanawake wajasiliamali vinavyotarajia kuanzishwa na Kanisa hilo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa