• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WAAJIRI KIGOMA WATAKIWA KUHESHIMU HAKI ZA WATUMISHI

Posted on: May 1st, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewaonya waajiri katika Sekta za Umma na binafsi mkoani hapa kuachana tabia ya kuwanyanyasa watumishi na kufuata Sheria na miongozo ya kazi wanazosimamia  ili kulinda haki na stahiki za watumishi walio chini yao.

Andengenye ametoa kauli hiyo alipozungumza na wafanyakazi wa Mkoa wa Kigoma  kwenye kwenye Hafla ya kilele cha maadhimisho ya Siku ya wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) iliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Mji Kasulu.

Amesema ni vizuri Menejimenti  za Taasisi zikajiwekea utaratibu wa kukutana na viongozi wa vyama huru vya wafanyakazi na kuweka mipango ya pamoja badala ya kuviona vyama hivyo kuwa ni maadui na kuvifanya kuwa daraja muhimu baina ya waajiri na waajiriwa.

Vyama vya wafanyakazi visibebe jukumu la kusimamia maslahi ya watumishi pekee bali vijikite pia katika kutoa Elimu, kusimamia kanuni na Sheria   kwa watumishi  sambamba na kujenga utaratibu wa kukutana mara kwa mara na pande zote mbili yaani waajiri na waajiriwa ili kutatua changamoto zinazojitokeza.

‘’mitazamo ya kujikita upande mmoja imekuwa ikichangia sana kukuza migogoro baina ya watumishi na waajiri wao hali inayosababisha uzoroteshaji wa matokeo chanya katika utendaji kazi na kushindwa kutoa huduma bora kwa wananchi’’ amesema.

Pia Andengenye amewataka watumishi kuendelea kupiga vita uvivu, rushwa, kuepuka vitendo vya utovu wa nidhamu, ubinafsi na kuongeza bidii na maarifa mapya katika utendaji kazi ili kuimarisha uchumi wao binafsi na maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine, mkuu huyo wa mkoa amewasisitiza watumishi wa Uma mkoani Kigoma kuendelea kuziamini taasisi rasmi za kifedha kwa kujiimarisha kiuchumi na kutimiza malemgo yao kupitia mikopo inayotolewa na Taasisi hizo huku akiwataka watendaji katika Taasisi hizo za kifedha kuendelea kupunguza riba za mikopo ili watumishi waweze kurejesha mikopo kwa muda muafaka.

Sambamba na hayo, Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha watendaji hao kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kushiriki zoezi la uchaguzi wa Serikali za mitaa ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha wananchi  kugombea nyadhifa mbalimbali katika nafasi za uongozi.

kadhalika amewaasa watumishi kuendelea kufanya mapinduzi ya kifikra sambamba na kuongeza juhudi, nidhamu na maarifa katika utendaji kazi wao wa kila siku.

Akisoma risala  kwa  mgeni rasmi Katibu wa Shirikisho la Vyama vya wafanyakazi mkoa wa Kigoma Jumanne Hamis ametoa wito kwa wafanyajkazi wote nchini kuongeza juhudi katika kufanya kazi zao huku wakizingatia weledi.

Kiongozi huyo ameiomba serikali kuwatazama upya baadhi ya wastaafu  kutokana na kulipwa kiasi cha fedha kisichoweza kukidhi mahitaji yao ya kimaisha huku akitoa ombi la  kwa serikali kuzielekeza Taasisi za kibenki  kupunguza riba katika mikopo wanayotoa kwa watumishi pamoja na kuchukua hatua kali kwa baadhi ya waajiri katika Taasisi binafsi kutokana na kushindwa kuzingatia sheria ya ulipaji wa mishahara kwa ngazi ya kima cha chini kuendana na miongozo.

Kadhalika ametoa pongezi kwa Mhe. Rais Samia Suluhu kwa kupandisha madaraja ya mishahara  kwa watumishi wa Umma, kuondolewa kwa tozo ya Asilimia Sita kwenye mikopo ya Elimu ya Juu, kuongeza  umri wa wategemezi kutoka miaka 18 hadi 21.

Aidha pongezi hizo zimehusisha serikali kushughulikia  maslahi ya watumishi walioondolewa kazini kwa kugushi vyeti pamoja na kulipa madeni ya mishahara ya walimu.

Kupitia hotuba hiyo, Katibu huyo ameiomba serikali kurejesha kikokotoo cha Asilimia Hamsini kwa moja chini ya mia tano arobaini kwa mshahara wa mwisho badala ya kutumia mfumo wa kutafuta mshahara bora wa miaka mitatu ya utumishi huku akisisitiza kufuatilia utendaji kazi wa mifuko ya hifadhi ya jamii kutokana na kushindwa kutekeleza wajibu wao wa kisheria wa kufuatilia michango ya watumishi kwa waajiri na kusababisha changamoto na mgogoro mkubwa baina ya mwajiri na mwajiriwa.

Maadhimisho ya Sikukuu ya Mei Mosi kimkoa kwa mwaka 2024 yanakaulimbiu isemayo ‘’Nyongeza ya Mishahara ni msingi wa kuongeza ufanisi na Tija katika utoaji wa Huduma na uzalishaji mali kwa ajili ya Maendeleo ya Jamii’’

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa