• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

Posted on: May 1st, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye  amevitaka vyama vya Wafanyakazi Mkoani hapa  kuwa daraja muhimu la kutatua changamoto baina ya waajiri na waajiriwa badala ya kuwa sehemu ya kuwachunguza, kuwashtaki na kuwanyanyasa watumishi wanaowawakilisha.

Amesema vyama hivyo vinapaswa kuzingatia usawa katika kusimamia haki za waajiri na waajiriwa ili kudumisha utendaji kazi wenye msingi wa kuleta matokeo chanya  kwa Umma na upatikanaji  wa maslahi kwa Watendaji.

Kauli hiyo ameitoa alipozungumza na maelfu ya wafanyakazi kutoka Taasisi za Umma na zile za Binafsi kwenye kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) kimkoa katika wilaya ya Kakonko mkoani hapa.

Amesema waajiri na waajiriwa wanapaswa kuendelea kuwa na uhusiano na ushirikiano mzuri kwani mahali popote pa kazi penye mahusiano mema, ujira mzuri na ulio halali lazima panakuwa na mafanikio na ufanisi katika uzalishaji au utoaji wa huduma.

Amesema wafanyakazi hususani katika Sekta za Umma wanapaswa kuongeza juhudi kiutendaji kazi kwani ni mashuhuda wa namna ambavyo Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyothamini utendaji kazi wao kwa kuendelea kubooresha maslahi yao ikiwa ni pamoja na kupandisha mishahara na madaraja katika ngazi mbalimbali za kiutumishi.

Kupitia hotuba yake, Andengenye amewataka wafanyakazi kujiimarisha katika matumizi ya Teknolojia pamoja na kujiwekea sera za kupambana na umasiki ili kutoa huduma bora na kuzalisha bidhaa zitakazomudu ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa  amewataka wafanyakazi mkoani Kigoma kushiriki kikamilifu mchakato wa uchaguzi kwa kujiandijisha na kupiga kura sambamba na kuihamasisha jamii kushiriki zoezi hilo kwa hali ya amani na utulivu.

Katika hatua nyingine Andengenye amemuagiza Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma kufuatilia na kuwasimamia waajiri wote ili kuhakikisha wanawasilisha michango ya watumishi  katika Mifuko ya hifadhi za jamii huku akiwataka waajiriwa kutumia Teknolojia kufuatilia hali ya uwasilishwaji na mapokezi ya michango hiyo.

Amesema kwa kufanya hivyo itawapunguzia usumbufu watumishi wanapotamatisha mikataba ya ajira katika mafao yao.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa