• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

VIJANA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA HALMASHAURI

Posted on: October 2nd, 2022

BAADHI YA MASHINE ZILIZOPO KATIKA KIWANDA KIDOGO CHA  VIJANA, KIKUNDI KAZI-IPOSA KILICJOPO MJINI KASULU.

Vijana wilayani Kasulu mkoani Kigoma wametakiwa kuchangamkia fursa ya Mikopo inayotolewa  na Serikali kwa makundi ya vijana, wanawake na walemavu, kutokana Asilimia Kumi ya Fedha inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri.

Kauli hiyo imetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Komredi Sahili Nyanzabala Geraruma, alipokagua na kuzindua Kiwanda kidogo cha vijana, Kikundi kazi-IPOSA kinachojishughulisha  na kazi za useremala na uchomeleaji wa vyuma kilichopo katika Halmashauri ya Mji Kasulu.

Amesema vijana wengi mitaani wanaujuzi wa kufanya kazi mbalimbali halali za uzalishaji lakini changamoto kubwa wanashindwa kufuata taratibu zilizowekwa na serikali ili kupata mikopo hiyo.

‘‘Nawashauri vijana wenzangu, bainisheni shughuli mnazotaka kuzifanya kwa ajili ya kujitafutia riziki kisha fuateni taratibu zinazotakiwa ili muweze kupata mikopo hiyo na mkajiinue kiuchumi’’

Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru  kitaifa, ameupongeza uongozi wa Serikali ya Mji wa Kasulu kwa ubunifu na usimamizi walioutoa kwa vijana hao, huku  akisisitiza  Halmashauri Kuendelea kutenga maeneo kwa ajili ya miradi ya Maendeleo ya vijana.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kasulu mjini ambaye pia ni Waziri wa Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu Prof. Joyce Ndalichako, amesema vijana wajitahidi kukopa kwa malengo na wahakikishe wanarejesha mikopo hiyo kwa wakati ili iweze kuwanufaisha wahitaji wengine wanaotaka kukopa.

‘‘Tuwe na malengo katika ukopaji wetu na tujitahidi kurejesha mikopo hiyo kwa wakati na itakapotokea tumeshindwa kurejesha basi tutoe taarifa kwa uongozi ili watupe utaratibu mzuri wa kufanya badala ya kukimbia deni’’

Nao vijana wa hao wa kikundi kazi-IPOSA, hawakusita kuishukuru serikali kwa kuwapa mkopo wa Fedha kiasi cha Shilingi Milioni mia moja ishirni na tano, Ushauri, Ardhi na Miongozo ya namna bora ya kutekeleza majukumu yao katika uendeshaji wa Mradi huo.

‘‘Mradi huu umetuheshimisha katika familia zetu na jamii kwa ujumla na kututoa katika orodha ya wazururaji na watu wasio na kipato cha uhakika, kwani kwa sasa tunaendesha maisha yetu vizuri na kutekeleza mipango mingine ya maendeleo’’ amesema Batholomeo Joel.

Mbio hizo za Mwenge wa Uhuru mkoani Kigoma zimehitimisha Siku ya Tano ambapo katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu, zimezindua  na kuweka jiwe la msingi jumla ya Miradi sita yenye Thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni Mia saba hamsini ikiwemo Mradi wa Maji Mganza, Barabara ya Lami Kumsenga, vyumba vitatu vya Madarasa katika shule ya Msingi Kumnyika, Nyumba ya watumishi wa Afya katika Zahanati ya Kijiji Mwibuye na Kikundi cha Vijana-IPOSA Kalema.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa