• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

UKATILI DHIDI YA WAJAWAZITO WATAJWA KUCHANGIA KUZALIWA WATOTO NJITI

Posted on: July 7th, 2023

MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. PHILIP MPANGO AKIJIANDAA KUKATA UTEPE KUASHIRIA RASMI MAPOKEZI YA VIFAA  TIBA  KUTOKA  TAASISI YA  DORIS MOLLEL FOUNDATION NA WADAU WAKE OREXY GAS PAMOJA NA TUME YA USHINDANI (FCC) KWA  HOSPITALI YA WILAYA BUHIGWE. WA KWANZA KULIA KWAKE NI DORIS MOLLEL, AKIFUATIWA NA MKUU WA MKOA WA KIGOMA MHE. THOBIAS ANDENGENYE.

MUASISI WA  TAASISI ISIYO YA KISERIKALI YA DORIS MOLLEL FOUNDATION BI. DORIS MOLLEL AKIZUNGUMZA  KWENYE HAFLA YA MAPOKEZI YA VIFAA TIBA VILIVYOTOLEWA NA TAASISI YAKE  KWENYE HOSPITALI YA  WILAYA  YA BUHIGWE JULAI 6,2023.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya wanawake wajawazito umekuwa ukichangia kuzaliwa kwa watoto njiti katika Jamii.

Dkt. Mpango ametoa kauli hiyo alipozungumza aliposhuhudia mapokezi ya vifaa Tiba pamoja na vitendea kazi kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe mkoani hapa.

Amesema uwepo wa changamoto kama mimba za utotoni, msongo wa mawazo, vipigo, ukosefu wa lishe bora, pamoja na tabia nyingine zisizo za kiutu wanazotendewa wanawake wajawazito,  kumechangia kusababisha baadhi yao kujifungua kabla ya wakati.

Amesisitiza kuwa, pamoja na uwepo wa sababu za Maradhi ya mfuko wa uzazi, mimba ya zaidi ya mtoto mmoja na magonjwa mbalimbali ya kuambukiza, wanawake wengi wamekuwa wakipatwa na tatizo hilo kutokana na changamoto za kimaisha zinazosababishwa na watu wa karibu ndani ya jamii.

Aidha, Dkt Mpango ameishukuru Taasisi ya Doris Mollel ikishirikiana na wadauwake  kwa kutoa msaada wa vifaa tiba vyenye Thamani ya Shilingi Mil. 190 katika Hospitali ya Wilaya ya Bihigwe zikiwemo Mashine 16 za kupima mapigo ya moyo, vitanda saba vya kujifungulia, viwili vya kupimia na vitatu vya kulalia wagonjwa.

Pia Taasisi hiyo imetoa magodoro 17, mashuka kumi, mashine mbili za kuzalisha hewa safi, hadubini moja na mashine 11 za kupima wingi wa damu.

Aidha Dkt. Mpango ameshuhudia ugawaji wa mitungi 300 ya Gesi iliyotolewa na kampuni ya Orexy Gas ya nchini, ambapo majiko214 yametolewa kwa wanawake wajawazito na16 kwa wasaidizi wa Afya.

Pia Makamu wa Rais Dkt. Mpango ameshudia mapokezi ya madawati 450 yaliyotolewa na Tume ya Ushindani nchini.

Awali akiwasilisha Taarifa ya ufadhili wa vifaa Tiba kwenye Hospitali ya wilaya Buhigwe, mwanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation Doris Mollel, amesema taasisi yake ilianzishwa mwaka 2015 ikilenga kusaidia Serikali kupunguza vifo vya watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya wakati (watoto njiti).

Amesema katika kipindi cha miaka 8, Taasisi ya hiyo imechangia vifaa Tiba katika Hospitali 64 nchini vikiwa na Thamani ya zaidi ya Shilingi Bil. 1.2.

Mollel amesema ‘’tumefanya utafiti kwa kushirikiana na Taasisi nyingine za nchi 11 Duniani, na kupitia utafiti huo taarifa iliyotolewa olibainisha  kuwa kila baada ya sekunde 2 mtoto anayezaliwa kabla ya wakati anapoteza maisha’’

 Ameendelea kusema kuwa, njia pekee ya kupunguza idadi ya vifo ni kutengeneza mazingira bora ya miundombinu ya kiafya kwa ajili ya kukabiliana na sababu za vifo hivyo pamoja na kuhakikisha jamii inaelimishwa ili  iweze kutambua na kuchukua hatua dhidi ya changamoto hiyo.

Molle amewahimiza wadau wa maendeleo na wote wanaoguswa na dhamira ya Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuendelea kuchangia kwa kutoa misaada mbalimbali kupitia Taasisi hiyo ili iweze kuendelea kuigusa jamii kupitia mpango wao wa  kunusuru maisha ya watoto njiti nchini.

 ‘’Mojawapo ya njia tunazotumia kupata fedha ni kupitia Matamasha mbalimbali ya michezo na burudani tukishirikiana na wanamichezo na wasanii maarufu, ambapo kupitia majukwaa hayo tunapata wasaa wa kukutana na wadau wetukwa lengo la kutuchangia fedha tunazoendelea kuzitumia kwa ajili ya kununua vifaa tiba’’ amefafanua Mollel.

Baadhi ya wakazi wa wilaya ya Buhigwe wameonyesha kuguswa na msaada huo huku wakiishukuru Taasisi ya Doris Mollel kwa kuwaletea mapinduzi ya kifikra kuhusu namna bora ya kuishi na kina mama wajawazito pamoja na kuepuka vitendo vinavyoweza kuwa visababishi vya uzazi wa watoto njiti.

Pia wanufaika waliopata ufadhili wa mitungi na majiko ya Gesi, wamesema msaada huo utawapunguzia adha ya kutumia muda mwingi kwa ajili ya kutafuta kuni.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa