• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

UJENZI NJIA YA UMEME NYAKANAZI KIDAHWE WAFIKIA 80%

Posted on: July 5th, 2024

UJENZI WA KITUO KIDOGO CHA KUPOZA UMEME KILICHOPO KIDAHWE JIRANI NA MJI WA KIGOMA

Ujenzi wa njia ya kusafirisha Msongo wa Umeme wa Kilovoti 400 kutoka Nyakanazi hadi Kidahwe wenye Thamani ya Shilingi Bilioni 434.9 umefikia zaidi ya 80% ambapo kukamilika kwa Mradi huo kunatajwa kuwa suluhisho la kudumu kutokana na mkoa kuwa na changamoto ya muda mrefu ya utoshelevu wa upatikanaji huduma ya Umeme.

Mradi huo unahusisha miradi mitatu ambapo kwa upande wa mradi wa ujenzi wa njia ya Umeme Nyakanazi hadi Kidahwe ulioanza kutekeleza Januari 2022 na Mkandarasi  M/s TATA Projects  Ltd  kutoka nchini India, umefikia 84% na unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 30, 2024.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu amedhamiria kuwaondolea wananchi wa mkoa wa Kigoma adha ya ukosefu wa umeme kwa kuidhinisha ujenzi wa mfumo huo utakaoingiza umeme wa kutosha na wenye uhakika katika kuendesha shughuli mbalimbali za uzalishaji mali.

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutaipunguzia hasara Serikali kwa kuachana na matumizi ya mafuta yanayofikia kiasi cha lita 30,000 kwa siku kwa ajili ya uendeshaji wa jenereta zinazozalisha Umeme unaotumika mkoani Kigoma,

‘’Matumizi ya jenereta yametupeleka kwenye mgao wa umeme kutokana na kutotosheleza kwa nishati hiyo, jambo lililochangia kwa kiasi kikubwa mkoa kukosa wawekezaji upande wa Sekta ya viwanda jambo linaloikosesha nchi kiasi kikubwa cha mapato’’ amesema.

Amefafanua kuwa, mpaka sasa mkoa umepokea maombi ya wawekezaji wenye nia ya kuwekeza kupitia sekta za viwanda ambao wanadhamira ya kuwekeza kutokana na kujihakikishia uwepo kwa umeme wa kutosha na wenye uhakika jambo litakalotoa fursa kwa wakazi kujipatia ajira za muda na zile za kudumu.

‘‘Ifahamike kuwa serikali inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa ya SGR kutoka Tabora hadi Kigoma yenye urefu wa Km. 506, ujenzi wa kiwanda cha kutengenezea Meli pamoja viwanda vingine vilivyopo vya kuchakata bidhaa mbalimbali ambavyo vyote hivyo vitahitaji kuendeshwa kwa kutumia  umeme wa uhakika’’ ameendelea kufafanua Andengenye.

Mhandisi wa ujenzi wa miundombinu ya Usafirishaji wa Msongo wa Umeme Nyakanazi hadi Kidahwe Nyango Magesa amesema kazi za usanifu wa mradi huo zimefikia 99% Manunuzi ya vifaa 99% pamoja na Ujenzi kufikia 84.4%.

mhandisi Magesa ameitaja miradi jumuish inayotekelezwa pamoja na mradi wa kusafirisha umeme Nyakanazi hadi Kidahwe kuwa ni pamoja na mradi ni ujenzi wa kituo cha kupoza  umeme KV 400/132/33 kilichopo mkoani Kigoma eneo la Kidahwe pamoja na upanuzi wa kituo cha kupoza Umeme Nyakanazi unaotekelezwa kwa thamani ya Shilingi Bil.164 na Mkandarasi M/s Sean and Hyuson kutoka Korea.

Ameutaja mradi mwingine unaotekelezwa sambamba na mradi huo ni ujenzi wa njia za usambazaji Msongo wa Umeme wa KV 33 na Voti 400 kwa Thamani ya Shilingi Bil. 11.5 ukitekelezwa na Mkandarasi M/s Giza Cable Industries kutoka nchini Misri pamoja na ujenzi wa Kituo cha kupoza Umeme Kigoma na Kasulu unaotekelezwa kwa Gharama ya Takribani Shilingi Bil. 9.2 ambapo hatua iliyofikiwa ni usanifu wa michoro, uchunguzi wa udongo kwa ajili ya kuona iwapo maeneo husika  yanafaa kwa ajili ya ujenzi wa miradi hiyo.

Mha. Magesa amesema ujenzi wa njia za usambazaji wa Umeme wa msongo wa kilovoti 33 na voti 400 utakapokamilika utavinufaisha vijiji vya Matendo, Kidahwe, Ngaraganza  na Matyazo wilaya ya Kigoma vijijini.

Vijiji vitakavyonufaika kwa wilaya ya Kasulu ni Makere, Nyachenda, Titye, Kitagata, Nyamidaho, Mvugwe, Nyarugusu, Muzye, Bugaga na Kasangezi ambapo kwa Halamshauri ya Mji ni Kanazi, Nyantare, Nyumbigwa na Bugaga.

Mhandisi Magesa amesema zoezi la ulipaji wa fidia kwa maeneo yaliyopitiwa na Mradi huo limekamilika kwa Asilimia 91 ambapo kiasi cha Shilingi Bil. 2.32 kimelipwa kwa wananchi ambao maeneo yao yamepitiwa na mradi na kwa wanaoendelea kuthibitisha taarifa zao watapokea malipo kabla ya mwishoni mwa Mwezi Agosti 2024.

Stephano Gwarema Mkazi wa Kijiji cha Rusesa amesema ameridhishwa na kasi ya serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo hususani suala la kuimarisha huduma za Umeme, Afya, Maji na barabara katika maeneo ya vijijini.

Kazi zinazoendelea kufanywa na serikali tumeridhishwa nazo na nitoe wito kwa wananchi wenzangu tuendelee kutunza miundombinu hii ili iweze kudumu kwa ajili ya matumizi ya sasa na vizazi vihavyo.

‘‘Mfumo huu wa Umeme unaotekelezwa mkoani Kigoma utakapokamilika utasaidia uwepo wa viwanda vitakavyoweza kutupatia ajira wakazi wa Kigoma na kujiimarisha kiuchumi ili tuweze kumudu kuendesha maisha’’ amesema Gwarema.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa