• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

TUTUMIE FURSA YA MABORESHO YA MIUNDOMBINU KUJIIMARISHA KIUCHUMI-RC ANDENGENYE

Posted on: April 26th, 2023

Ikiwa ni Kilele cha Maadhimisho ya Miaka 59 ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar, Wananchi mkoani hapa wametakiwa kuendelea kutumia fursa ya uwepo wa maboresho makubwa ya Miundombinu ili kujiimarisha kiuchumi na kujiletea Maendeleo wao binafsi na mkoa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye alipozungumza na wakazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Leo Aprili 26, 2023 kwenye Kilele cha Wiki ya Maadhimisho ya Muungano.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya Ujenzi wa Miundombinu pamoja na kuimarisha mifumo ya utoaji na upatikanaji wa Huduma za Jamii mkoani hapa kwa ajili ya Maendeleo ya Wananchi.

‘’Serikali inatekeleza Ujenzi wa Meli za uchukuzi wa watu na mizigo katika Ziwa Tanganyika pamoja na ukarabati wa Meli tatu zilizokuwa zikitumika awali, pia imeendelea kuimarisha miundombinu ya usafirishaji ikiwa ni pamoja na manunuzi ya mabehewa mapya 20 Treni ya Reli ya Kati na kuanza ujenzi wa Reli ya kisasa ya SGR’’

‘’Mkataba wa uboreshaji wa uwanja wa ndege wa Kigoma ulishasainiwa na kazi zikikamilika zitauwezesha uwanja kupokea ndege nyakati zote, kuhudumia abiria laki nne kwa Mwaka pamoja na kurefusha uwanja hadi kufikia Km 3’’ amesema.

Upande wa Nishati ya Umeme Andengenye amefafanua kuwa, Serikali inatekeleza mradi mkubwa wa Umeme utakaoingiza kiasi cha Kv 400 kutoka Nyakanazi hadi Kidahwe, pamoja na miradi mingine miwili ambayo itauunganisha Mkoa na Gridi ya Umeme kutoka Tabora na Mpanda.

‘’Ongezeko la kiwango cha Umeme litawavutia wawekezaji hususani wanaotaka kuanzisha viwanda kutokana na hapo awali Mkoa kukosa Umeme wa kutosha na wenye uhakika hivyo kuunyima fursa ya uanzishwaji wa viwanda vikubwa na vidogo’’ ameongeza.

Aidha Mhe. Andengenye amewapongeza viongozi wakuu wa Serikali wa Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuwaletea Maendeleo wananchi chini ya Muungano wa Serikali hizo mbili.

Pia Mkuu wa Mkoa ametumia fursa hiyo kuwaasa wakazi wa Wilaya ya Buhigwe kuutunza Mradi wa Maji ambao ameuwekea jiwe la Msingi kuelekea kilele cha Maadhimisho hayo uliopo katika kijiji cha Songambele wilayani humo.

Rai yangu kwenu, Mradi huu umeigharimu Serikali zaidi ya Shilingi Bil.1.6 hivyo hakikisheni mnaitunza miundombinu yake ili idumu na muweze kupata huduma hiyo kwa muda mrefu zaidi.

‘’Suala la kuchangia gharama za uendeshaji ni jambo la kawaida, hivyo ili kupata uendelevu wa huduma hii tunahitaji kulipia gharama za matumizi ya huduma ya maji ili kuwawezesha wasimamizi pamoja na kufanya manunuzi ya vifaa vinapoharibika’’ amesisitiza Andengenye.

Awali akiwasilisha Taarifa ya Ujenzi wa Mradi wa Maji kwa vijiji vya Buhigwe, Kavomo, Mlera na Bwega, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Buhigwe Mha. Gideon Katoto amesema mradi huo utakapokamilika unatarajia kunufaisha wakazi 14,378 wa vijiji hivyo.

Amefafanua kuwa Tanki lililojengwa linaujazo wa lita 500,000 huku chanzo cha Maji kikiwa na uwezo wa kuzalisha lita 1,994,500 kwa siku huku uhitaji wa Maji katika vijiji hivyo ukiwa ni lita 380,600 kwa Siku.

‘’Mradi huu kwa sasa umefikia Asilimia tisini na kazi zilizobaki za ulazaji wa mabomba ili kuwafikishia wananchi huduma inaendelea, aidha ukarabati wa matanki mawili katika vijiji vya Kavomo na Mulera umekamilika’’ amesisitiza Mhandisi Katoto.


PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA MAADHIMISHO YA KIMKOA YA SHEREHE ZA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR WILAYANI BUHIGWE LEO APRILI 26, 2023.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa