• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

TUMIENI MFUMO WA TAUSI KUFANYA MAKUSANYO YA HALMASHAURI -ANDENGENYE

Posted on: June 7th, 2023


Mkuu wa  Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye (kushoto) akimsikiliza Meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji  Mhe. Baraka Lupoli (katikati) aliposhiriki Mkutano wa Baraza la Madiwani katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa ajili ya kupikea na kujadili Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali  kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Juni 30, 2022. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Kigoma/Ujiji Athumani Msabila.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amepiga marufuku Halmashauri zote mkoani Kigoma kutumia mifumo tofauti na ule wa  TAUSI katika kufanya makusanyo ya ndani kwenye  Halmashauri hizo.

Andengenye ametoa Maelekezo hayo Juni 6, 2023 wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Madiwani Manispaa ya Kigoma/Ujiji kujadili Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha unaoishia Juni 30, 2022.

Mkuu wa Mkoa amesema kitendo cha kutumia mifumo ya zamani ya ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ikiwa ni pamoja na matumizi ya Risiti kinaendelea kutoa mianya ya kufanyika kwa urasimu kwa baadhi ya watendaji wasio waaminifu.

‘’Kupitia Baraza hili ninatoa Maagizo kuwa ni marufuku kwa watendaji katika Halmashauri zote mkoani hapa kutumia au kuidhinisha matumizi ya mifumo tofauti na huu uliorasimishwa na Serikali katika kukusanya mapato ya ndani na watakao kaidi na kwenda kinyume watakuwa wanakiuka Maelekezo ya Serikali kwa makusudi na hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao’’ amesema.

Ameongeza kuwa, mfumo wa Tausi unawafanya wananchi kuwa na Imani kuwa malipo wanayoyafanya yanakwenda sehemu sahihi badala ya baadhi ya watu kutunza Fedha za Serikali kwenye mifuko yao na kuziwasilisha kwa muda wanaotaka.

Akitoa maelekezo kuhusu utekelezaji wa Taarifa ya  Mkaguzi wa ndani kwa Halmashauri hiyo, Mkuu wa Mkoa amesisitiza Baraza hilo la Madiwani kwa kushirikiana na watendaji wa Halmashauri kuchukua hatua za kinidhamu kwa watumishi watakaobainika kuhusika  na vitendo vya ubadhirifu na kusababisha Manispaa hiyo kukosa mapato kama ilivyokusudiwa.

‘’Nasisitiza uchukuaji wa hatua uhusishe watumishi wote wenye ajira za kudumu na wale wenye mikataba  ili kuimarisha uwajibikaji kwenye usimamizi wa Fedha na Rasilimai nyinginezo za Serikali  ili kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato’’ amesisitiza Andengenye.

Pia kiongozi huyo amewataka Madiwani katika Halmashauri zote mkoani hapa kuzingatia kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma katika utendaji kazi wao.

‘’Epukeni matumizi mabaya ya Madaraka kupitia nafasi zenu, hii itawasaidia wananchi kuwaamini katika maamuzi mnayoyafanya na kuondoa malalamiko yasiyo na msingi katika jamii mnayoiongoza’’ ameshauri Andengenye.

Naye Meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Baraka Lupoli amesema upungufu wa watumishi katika Idara ya Fedha na Biashara katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji unachangia kwa kiasi kikubwa kupotea kwa mapato ya ndani hali inayosababaisha makusanyo kukusanywa chini ya kiwango.

‘’Makadirio ya makusanyo yetu kwa Mwezi ni zaidi ya Shilingi Mil. 400 ila kutokana na changamoto hizo, makusanyo yetu hushuka hadi kufikia kiasi cha Shilingi Mil. 270 kwa Mwezi’’ amesisitiza Mhe. Meya.

Kwa upande wao Madiwani wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji wameiomba Serikali kutafuta suluhisho la changamoto ya uhaba wa watumishi katika Idara ya Fedha na Biashara ili kuongeza tija na ufanisi katika ukusanyaji wa mapato.

Upungufu wa  watumishi kwa sasa umesababisha Halmashauri  hiyo kutumia wakusanya mapato wenye Ajira za mikataba ambao baadhi yao wamekosa uaminifu na kusababisha upotevu mkubwa wa mapato katika Halmashauri hiyo.

Kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji imepata Hati Safi ya ukaguzi wa Hesabu za Serikali.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa