• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

TOENI TAARIFA YA MIRADI MNAYOITEKELEZA KWA WANACHI ILI KUONDOA SINTOFAHAMU- MHE. ANDENGENYE.

Posted on: December 14th, 2022

Wakuu wa Taasisi za Serikali zinazotekeleza Miradi ya Barabara mkoani Kigoma wametakiwa kujenga tabia ya kutoa taarifa za miradi wanayoisimamia na kuitekeleza kwa ili wananchi wawe na uelewa kuhusu kazi zinazofanywa na Serikali pamoja na kuwajengea uwezo wa kufuatilia na kuhoji kuhusu kazi hizo.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye alipokuwa akifungua kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa kilichofanyika leo Tarehe 14 Desemba 2022 katika Ukumbi wa NSFF Manispaa ya Kigoma/Ujiji.

‘’Kupitia viongozi wa ngazi mbalimbali za kisiasa, tunaweza kufikisha ujumbe kwa Wananchi ili waweze kufahamu kiasi cha Fedha kinachotolewa na Serikali kisha kuelekezwa kwenye Miradi ya Barabara. Pia wataweza kutambua aina ya Miradi inayotekelezwa pamoja na hatua zilizofikiwa. Hii itawaongezea ufahamu kujua miradi inayotekelezwa na kuondoa maswali yasiyo ya lazima’’ alisema.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa matengenezo ya barabara 2021/2022 na 2022/2023, Miradi ya maendeleo na ahadi za viongozi,  Meneja wa Wakala wa Barabara Mkoa Mha. Narcis Choma amesema mtandao wa Barabara unaohudumiwa na wakala huyo kimkoa unajumla ya Kilomita 1,547.03 ambapo Barabara kuu ni Km. 753.63 na Barabara za Wilaya ni 135.5.

Amefafanua kuwa, upande wa Madaraja wanahudumia Jumla ya madaraja 381 yaliyopo barabara kuu yakiwa 130 na za Mkoa 251. Aidha amesema matarajio ni kuongeza utoaji wa huduma za barabara na madaraja kuendana na upatikanaji wa Fedha ili kuondoa kero hiyo kwa wananchi.

Upande wake meneja wa Wakala wa Barabara za vijijini na Mjini Mkoa Mha. Godwin S. Mpinzile, amesema wataendelea kuzibainisha na kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali za barabara ili kuhakikisha maeneo mengi ya Mkoa yanapitika na kufikika kwa urahisi.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa