• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

THPS YAKABIDHI HADUBINI TANO KUKABILIANA NA UGONJWA WA KIFUA KIKUU

Posted on: June 22nd, 2023

Shirika la Tanzania Health Promotion Support (THPS) limekabidhi Hadubini Tano zenye Thamani  ya Shilingi Mil. 35 kwa ajili ya kuimarisha Huduma za uchunguzi wa kimaabara katika Vituo  vinavyotoa Huduma ya Upimaji wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu mkoani Kigoma.

Mara baada ya Kupokea Hadubini hizo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Jesca Leba amelishukuru Shirika  la THPS na kusisitiza kuw,a vitendea kazi hivyo vitapanua wigo wa Matibabu ya  Maradhi ya Kifua Kikuu mkoani Kigoma.

Dkt. Leba amesema vifaa hivyo vitaongeza kiwango cha ugunduzi wa Magonjwa ya kifua Kikuu pamoja na kusaidia kutambuliwa kwa wagonjwa katika hatua za awali na kuruhusu kuanza matibabu ya mapema kabla ya kuathirika zaidi.

 ‘’Tunawashukuru THPS kwani ufadhi wa vitendea kazi hivi ambavyo vitaongeza Idadi ya vituo vya kupimia wagonjwa pamoja na kusogeza huduma hii muhimu karibu na Wananchi’’ amesema Dkt. Leba.

Naye Meneja wa Kanda wa Mradi wa THPS Dkt. Benedict Nyilo, amesema Hadubini hizo zitagawiwa katika vituo vitano vya Uchunguzi wa Kifua kikuu kwenye Halmashauri za Wilaya Kakonko, Kasulu, Uvinza na Manispaa ya Kigoma/Ujiji.

‘’Tunatambua na kuthamini Dhamira ya Serikali katika kukabiliana na kutokomeza kabisa ugonjwa wa Kifua Kikuu nchini ifikapo Mwaka 2030, hivyo tumetoa vifaa hivi kwa lengo la kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuukabili ugonjwa huo’’ amesema Dkt. Nyilo.

Dkt. Nyilo amewataka Wananchi kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kupima Afya zao wanapobaini dalili za ugonjwa huo, kwani vipimo vinatolewa bure ikiwa ni mkakati wa Serikali katika kuyakabili maradhi hayo.

Naye Mtaalam kutoka Maabara Kuu ya kudhibiti Maradhi ya Kifua Kikuu na Ukoma ya Jijini Dar es Salaam, Said Mfaume, amesema hadubini hizo zitaongeza kasi katika uibuaji wagonjwa wapya wa Kifua Kikuu mkoani Kigoma.

Ameendelea kusisitiza kuwa, kupatikana na Hadubini hizo kutaongeza Idadi ya Vituo vya kutolea Huduma za Upimaji wa ugonjwa wa Kifua Kikuu mkoani Kigoma na kuifikia idadi kubwa ya walengwa katika kupambana na ugonjwa huo.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa