• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

TASAC KUENDELEA KUIMARISHA UTENDAJI KAZI BANDARI YA KIGOMA

Posted on: March 27th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye ameupongeza Uongozi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kwa  kusimamia shughuli za bandari kwa ufanisi jambo linaloendelea kuimarisha usalama na ukuaji wa uchumi wa nchi.
Andengenye ametoa pongezi hizo alipotembelewa na Afisa Mfawidhi wa TASAC Mkoa wa Kigoma, Adam Mamilo aliyefika ofisi ya Mkuu wa Mkoa  kwa lengo la kujitambulisha mara baada  kuwasili katika kituo chake kipya cha kazi Mkoani hapa.Amesema TASAC  inapaswa kuongeza nguvu katika kuboresha huduma za usafirishaji majini hususani katika bandari ya Kigoma kutokana kasi ya serikali kufanya maboresho makubwa ya miundombinu mkoani hapa, hali inayovutia wafanyabiashara wengi kutoka ndani na nchi jirani za Burundi, Kongo DR na Zambia kutumia bandari hiyo.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema  fursa za kiuchumi zitokanazo na Ziwa Tanganyika zimechangia ongezeko kubwa la vyombo vya uchukuzi visivyo rasmi vinavyochangia kuhatarisha usalama wa wananchi wanaovitumia, hivyo serikali kwa kuliona hilo imeamua kuwekeza katika uboreshaji miundombinu ya uchukuzi ikiwemo ukarabati wa Meli ya Mt. Sangara, Mv Liemba pamoja na Mv. Mwongozo.

"Nitoe Rai kwa uongozi wa TASAC mkoa wa Kigoma kwenda kusimamia na kuhakikisha ukarabati wa meli hizo unakamilika kwa wakati ili tuweze kukabiliana na mahitaji makubwa ya usafirishaji wa watu na bidhaa za kibiashara huku  tukiimarisha usalama wa maisha ya watu na mali zao katika ziwa Tanganyika" amesema.

"Kwa sasa tayari mkoa umeunganishwa na Bararara ya Lami kutoka Kigoma kwenda mikoa ya Kagera na Shinyanga huku upande wa Tabora ujenzi ukiwa katika hatua za mwisho  na kwa upande wa Katavi ujenzi unaendelea vizuri, hii inazidi kuchangia ongezeko la wawekezaji ambao pia watatumia bandari kusafirisha bidhaa na kuongeza mzigo wa utendaji kazi wa bandari ya Kigoma" ameeleza Rugwa.

Upande wake Afisa Mfawidhi wa TASAC Kigoma Adam Mamilo ameahidi kushirikiana na viongozi wa Serikali ya Mkoa kwa ajili ya kupokea ushauri utakaolenga kuhakikisha miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi wa Bandari inakamilika kwa wakati.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa