• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

TARURA YAAGIZWA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA WAVAMIZI KATIKA HIFADHI ZA BARABARA

Posted on: May 16th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye ameuelekeza Uongozi wa Wakala wa Barabara za Vijijini  na Mjini (TARURA) Mkoa wa Kigoma kuchukua hatua za kisheria dhidi Taasisi au mtu yoyote anayetekeleza shughuli za kibinaadamu katika maeneo tengefu ya Hifadhi za Barabara ili kuruhusu yaweze kutumika kama ilivyokusudiwa na Serikali.

Mkuu wa Mkoa ametoa maelekezo hayo kufuatia athari zinazoendelea kujitokeza kutokana na baadhi ya wakazi kuvamia Hifadhi za barabara na kufanya shughuli mbalimbali za kibiashara, Kilimo, kuchunga mifugo pamoja na uchimbaji wa mchanga  hali inayosababisha uharibifu  wa miundo mbinu hiyo.

‘’Serikali inatumia kiasi kikubwa cha fedha kuboresha miundombinu hii muhimu ya usafirishaji lakini baadhi ya watu wamevamia na kuanzisha Karakana kwa ajili ya kutengeneza magari na pikipiki, ujenzi wa vibanda vya Biashara, kufanya shughuli za kilimo, pamoja na uchimbaji wa mchanga hususani nyakati za mvua au katika maeneo yenye madaraja’’ amesema.

Pamoja na shughuli hizo kuathiri barabara na kusababisha msongamano kwa baadhi ya maeneo, Andengenye ametoa Tahadhari ya uwezekano wa kutokea vifo au majeruhi kwa watu wanaovamia hifadhi hizo kutokana na ajali zinazoweza kusababishwa na vyombo vya usafiri kuacha njia na kuwafikia kwa wepesi.

‘’Hatukatazi watu kutafuta riziki lakini pia utafutaji huo uende sambamba na uzingatiaji wa Sheria za nchi na Usalama wetu, kwani Serikali ilishatenga maeneo rasmi kwa ajili ya shughuli za kibiashara lakini baadhi ya watu wanaamua kupuuza kwa makusudi na  kuendelea kuendesha shughuli za kiuchumi katika maeneo yasiyo sahihi’’ Amefafanua Andengenye.

Aidha Andengenye amesisitiza kuwa, maboresho makubwa ya Miundombinu ya Barabara yanayoendelea kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita yaende Sambamba na muitikio wa wananchi katika kujiimarisha kiuchumi ili kukabiliana na wimbi kubwa la wawekezaji kutoka nje ya Mkoa wa Kigoma wanaoanza kuzitazama na kuchangamkia fursa zilizopo kufuatia mkoa kuzidi kufunguka kibiashara.

‘’Uwepo wa Miundombinu rafiki ya uchukuzi na usafirishaji pamoja na Serikali kuendelea kuuimarisha hali ya utoshelevu wa Umeme , vitaongeza  kasi ya uwekezaji na ushindani wa kibiashara sokoni  kutoka kwa wawekezaji mbalimbali wa nje ya Mkoa, hivyo sisi wenyeji tunapaswa  kuwa wa kwanza kuchangamkoa fursa zilizopo’’ amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Upande wake Meneja wa TARURA Wilaya ya Kigoma Mha. Elias Mutapima amesema changamoto wakazi kufanya uharibifu mkubwa wa mitaro, kutupa taka ovyo zinazosababisha mitaro kuziba na hata kupasuka pamoja na kushusha vifaa vya ujenzi katika maeneo ya barabara.

Ameendelea kueleza kuwa, matumizi mabaya ya hifadhi za Barabara katika uwekaji wa miundombinu mingine kama ile ya Umeme  na Maji vimeendelea kusababaisha kuchelewa kukamishwa kwa baadhi ya miradi na kuendelea kuwepo kwa adha ya ukosefu wa barabara zenye ubora katika baadhi ya Maeneo katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji.

''Ili kukabiliana na Changamoto hizi, tunajitahidi kujenga mitaro na makaravati ili kudhibiti Barabara zisiharibiwe na Maji ya Mvua, kuendelea kutoa Elimu ya utunzaji wa Barabara pamoja na kushirikiana na wataalam wenzetu ili kuhakikisha tunahamisha kwa haraka miundombinu iliyowekwa kwa makosa kwa lengo la kuharakisha ufikishaji wa huduma kwa Wananchi'' ameeleza  Mha. Mutapima.

PICHA; Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye (Kushoto) akipokea  na kupitia taarifa ya utekelezaji wa Ujenzi wa miradi ya Barabara  zinazosimamiwa na TARURA katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji, kutoka kwa Meneja wa TARURA  Wilaya ya Kigoma Mha. Elias Mutapima(Kulia)

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye akiburudika na kinywaji aina ya Kahawa huku akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza alipotembelea wilaya hiyo kwa lengo la kukagua utekelezaji wa Ujaenzi wa Miradi ya Barabara zilizo chini ya TARURA.

PICHA: Muonekano wa Baadhi ya Barabara zilizotembelewa na Mkuu wa Mkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza pamoja na Manispaa ya Kigoma/Ujiji

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye akizungumza na wakazi wa Kata ya Mwandiga katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji akiwa katika ziara yake ya kukagua Miradi ya Ujenzi wa Barabara.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa