• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

TANZANIA NA CONGO DR ZAWEKA MKAKATI KUKABILIANA NA MAJANGA

Posted on: February 21st, 2024

Kamati za Maafa kutoka Mkoa wa Kigoma pamoja na mikoa ya Kivu Kusini na Tanganyika katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo zimekutana kwa lengo la kubadilishana mbinu, kujadili na kuweka mikakati ya pamoja yenye lengo la kukimarisha njia za kukabiliana na majanga katika ukanda huo.

Akifungua Mkutano uliozikutanisha pande hizo na kufanyika tarehe 20-21, Februari 2024 katika Ukumbi wa NSSF Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mkuu wa Mkoa wa KigomaThobias Andengenye amesema athari za majanga huwa hazina mipaka kijiografia hivyo ni jambo jema kwa pande hizo kukaa chini na kuweka mikakati ya pamoja yenye lengo la kuepuka au kupunguza athari zinazoweza kuyakumba maeneo hayo na kuleta madhara kwa wakazi.

Ameyataja majanga yanayoendelea kuleta athari mara kwa mara katika maeneo hayo kuwa ni ukosefu wa Amani, uwepo wa magonjwa ya mlipuko, ongezeko la wakimbizi, uharibifu wa mazingira, mafuriko, kuongezeka kwa kina katika ziwa Tanganyika pamoja na uwepo wa ajali za marakwa mara katika ziwa hilo.

Kupitia kikao hicho, mkuu huyo wa mkoa amezitaka Kamati hizo kuhakikisha zinaweka mikakati ya kudumu katika kushughulikia majanga hayo ili kupunguza athari ikiwemo vifo, ukosefu wa Amani katika nchi ya Congo unaochangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira pamoja na mdororo wa kiuchumi katika ukanda huo.

Upande wake Mratibu wa Shirika lisilo la kiserikali la REDESO Mkoa wa Kigoma Emmanuel Solomon amesema kamati hizo zinakabiliwa na changamoto za udhaifu kwenye usimamizi wa Sheria na miongozo inayotungwa na nchi husika za Tanzania na Congo DR.

Amezitaja changamoto nyingine kuwa ni ongezeko la wahamiaji haramu kutoka nchi ya Congo na kuingia Tanzania kinyume cha Sheria,  ufinyu wa bajeti kwa ajili ya kuziwezesha kamati hizo kufanya ufuatiliaji sambamba na uelewa mdogo wa wakazi katika maeneo hayo kuhusu athari za majanga ili kushiriki kuchukua tahadhari.

Solomon amesema baadhi ya mapendekezo ya jumla waliyoyafikia kupitia kikao hicho ni pamoja na kuzitaka Serikali za pande zote mbili kutilia mkazo na kufuatilia kwa karibu mikakati ya kukabiliana na majanga, kuhakikisha mikakati hiyo inatekelezwa kwa vitendo sambamba na kuziwezesha kamati kifedha ili zimudu kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Akifunga Mkutano huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali  Michael Ngayalina ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe ametoa wito kwa Kamati hizo kushirikiana na mamlaka husika za serikali zao ili kuchukua hatua za muda mrefu katika kukabiliana na majanga.

Aidha Kanali Ngayalina amewashukur wadau wote waliofanikisha kufanyika kwa Mkutano huo na kusisitiza kuwasisitiza wajumbe kuhakikisha maazimio yaliyofikiwa yanafanyiwa kazi kwa ufasaha.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa