• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SHULE SHIKIZI ZASAIDIA WATOTO KUPATA ELIMU MKOANI KIGOMA

Posted on: December 6th, 2017


Suala ala utoaji elimu si jambo la serikali tu bali ni ushirikiano wa sekta binafsi, jamii na serikali kwa pamoja zinaweza kuleta mabadiriko makubwa ya kimaendeleo kieleimu.

umbali kutoka maeneo wanayoishi jamii na sehemu inakopatikana huduma ya elimu imekuwa ni changamoto kwa baadhi ya maeneo hususani vijiji ambapo jamii nyingi hasa za wakulima na wafugaji huishi kwa kuhamahama kufuata huduma za mashamba ya kilimo na malisho ya mifugo jambo amabalo hufanya jamii hizi zikae mbali na huduma za kijamii kama vile elimu, afya, usafiri.

Kijiji cha Kazage katika kata ya Shunguliba Wilayani Kasulu ni moja ya Kijiji ambacho kimepambana na  changamoto ya kuwa mbali na maeneo ya upatikanaji wa huduma za kijamii, suala lililopelekea watoto wengi kukosa fursa ya kupata elimu ya msingi.

Kijiji cha Kazage kipo umbali wa kilomita 10 hadi kufikia huduma ya elimu elimu ya msingi iliyopo katika kijiji jirani cha Shunguliba. Kutokana na umbali mrefu, asilimia 100 ya watoto wenye umri wa kwenda shule hushindwa kupata elimu.

Shirika la EQUIP Tanzania linalojishugulisha na mpango wa kuinua ubora wa elimu, ndilo limekuwa msaada katika kijiji cha Kizage kwa kuwaokoa watoto walioshindwa kupata elimu ya msingi likaja na mpango wa kusaidia uanzishwaji wa ‘Shule Shikizi’.

Shule shikizi zinatokana na shule mama zilizopotayari na zenye miundombinu kamili, shule hizi hujengwa ili kusaidi watoto waliokosa fursa ya masomo ya awali.

Kutokana na uhitaji wa elimu EQUIP Tanzania imeweza sasa kusidia ujenzi wa madarasa mawili ya shule shikizi katika kijiji cha Kizage, ujenzi wa madarasa mawili hadi sasa umesaidia watoto kupata elimu kwa asilimia.

Mtendaji wa Kijiji cha Kizage Bw. Timoth Zabronia anatoa ushuhuda wa faida za shule shikizi namna zilivyosaidia kuinua elimu kijijini hapo akisema “watoto wet hapa walikuwa wengi hawasomi kutokana na umbali mrefu hadi kuifikia shule mama iliyopo Kijiji cha shunguliba, sasa tunashukuru mradi wa EQUIP Tanzania kwa kuona umuhimu wa watoto wetu kupata elimu kupitia shule hizi shikizi sasa watoto wengi wameanza kupata elimu ya awali na hatimaye kuendelea na darasa la kwanza”

Wananchi wa Kizage wanato shukrani na pongezi kwa mradi wa EQUIP Tanzania ambayo imekuwa ikiwahamasisha kujenga maboma ya madarasa na kasha kusaidia hatua ya upauaji na samani za madarasa, kwa nguvu hii, wakazi wa Kizage wameweza kufyatua tofali kwa nguvu zao na kujenga madarasa mawili pamoja na ofisi ya walimu katika shule shikizi ili kuondokana na adha ya kukosa elimu watoto wao.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa