• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SHUGHULI ZA KIBINADAMU CHANZO CHA ONGEZEKO LA KINA CHA MAJI ZIWA TANGANYIKA

Posted on: March 21st, 2024

Shughuli za kibinadamu pamoja na changamoto za uwepo wa majanga ya Asili zimetajwa kuwa sababu ya kuongezeka kwa kina cha maji katika Ziwa Tanganyika.

Hayo  yamebainishwa kupitia mawasilisho ya Mkutano wa Mwaka wa Kamati za kukabiliana na majanga katika mkoa wa Kigoma na mikoa jirani ya nchi ya Burundi uliofanyika katika Ukumbi wa NSSF, Manispaa ya Kigoma Ujiji, mjini hapa.

Imebainishwa kuwa tafiti zilizofanywa zimeonesha athari za majanga ya Asili ikiwemo milipuko ya Volkano katika baadhi ya milima nchini Congo DR, imesababisha lava iliyopoa pamoja na udongo kuingia katika mto Lukuga na kuzuia maji kupita kwa ufanisi ili kuingia katika bahari ya Atlantic.

Aidha kupitia mkutano huo, imebainika kuwa ongezeko la shughuli za kibinadamu pembezoni mwa mto Lukuga,  zinasababisha mmomonyoko wa ardhi  hivyo mchanga huingia katika mto huo na kutoruhusu maji kupita kwa ufanisi kutoka Ziwani na kuingia baharini.

Baadhi ya athari zilizotajwa kujitokeza kutokana na changamoto ya kuongezeka kwa kina cha maji katika ziwa hilo ni pamoja na Maji kujaa katika maeneo yaliyojengwa miundombinu hususani bandari, makazi, kupotea kwa fukwe, uwepo wa mafuriko kutokana na mito kushindwa kuingiza kungiza Maji Ziwa Tanganyika na kusababisha uharibifu wa makazi pamoja na mashamba.

Katika hatua nyingine wajumbe wa kikao hicho wameafikiana kuushauri uongozi wa serikali za Tanzania, Burundi na Congo DR kuweka mikakati mipya ya udhibiti wa shughuli za kibinadamu zinazosababisha uharibifu wa mazingira katika ziwa hilo na maeneo jirani ikiwemo kuongeza kasi katika usimamizi wa matumizi bora ya ardhi.

Aidha, katika kukabiliana na majanga kikao hicho kimeainisha changamoto zinazokinzana na juhudi za kufikia malengo ya kamati hizo ikiwemo ufinyu wa bajeti, wakazi kukosa elimu ya kukabiliana na majanga, uharibifu wa Mazingira, uhamiaji haramu pamoja na matumizi hafifu ya Teknolojia katika kukabili majanga.

Sambamaba na hayo, wajumbe wa mkutano wamekubaliana kwenda kusimamia uzingatiaji wa mikakati ya pamoja iliyowekwa  kwa ajili ya kukabiliana na majanga kwa kuishusha ngazi za chini ili iweze kutekelezwa na wananchi  ambao ndio walengwa.

Ongezeko la maji katika ziwa Tanganyika, uhamiaji holelea wa wakazi wa maeneo hayo kwa lengo la kutafuta fursa za kimaisha na usalama, milipuko ya magonjwa pamoja na uharibifu mkubwa wa Mazingira  vikiainishwa na mkutano huo kuwa ni sehemu kubwa ya majanga yanayowakabili wakazi katika mkoa wa Kigoma na mikoa jirani ya nchi za Congo DR na Burundi.

Mkutano huo wa wadau hao wa majanga umefadhiliwa na Mashirika yasiyo ya kiserikali ya REDESO na Help Age Tanzania kwa lengo la kuunga mkono kuhamasisha utayari na kuunda mfumo wa pamoja wa tahadhari katika kukabili majanga kwa mikoa hiyo jirani katika nchi hizo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa