• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SERIKALI YATOA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA MAAFA KWA WATENDAJI NA WENYEVITI WA VIJIJI KIGOMA DC

Posted on: August 26th, 2024

Katika kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imesema itaendelea kuweka mikakati na kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kutoa mafunzo ya kukabiliana na Maafa yanayoweza kujitokeza ili kupunguza athari zake kwa wananchi mkoani Kigoma na Tanzania kwa ujumla.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Dkt. Salum Manyata alipozungumza kwenye semina ya kujenga uelewa juu ya upunguzaji wa madhara ya Maafa katika Jamii iliyofanyika katika Halmashauri ya wilaya ya Kigoma iliyowahusisha wenyeviti wa vijiji, watendaji kata na vijiji pamoja na Maafisa kutoka Halmashauri hiyo na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Amesema mafunzo hayo yamewalenga viongozi hao kwa kuwa kundi hilo lipo karibu sana na wananchi wanaoguswa moja kwa moja na majanga hivyo ushiriki wao utarahisisha kufikisha maarifa hayo kwa wananchi sambamba na kushusha mipango ya kukabiliana na majanga katika ngazi hizo.

‘‘Kupitia semina hii tumewaelekeza namna bora ya kushughulika na majanga kabla, wakati na muda mfupi baada ya majanga kutokea sambamba na kubaini vihatarishi, vilivyopo katika maeneo yao, namna bora ya kutoa taarifa katika mamalaka za juu pamoja na kutoa elimu kwa jamii’’ amesema Dkt. Manyata.

Amesema miongoni mwa sababu za majanga zilizobainishwa na wananchi kupitia washiriki hao kuwa ni pamoja na baadhi ya wakazi kujenga makazi yao katika maeneo yenye miteremko mikali, ujenzi pembezoni mwa ziwa Tanganyika, uwepo wa upepo mkali, mvua za mawe na mmomonyoko wa udongo.

‘‘Mara baada ya kuwajengea uwezo, washiriki hawa wanapaswa kutengeneza mipango ya pamoja itakayoisaidia kamati elekezi ya wilaya na mkoa kuitekeleza mipango hiyo kwa lengo la kuchukua tahadhari au kupunguza athari zinazoweza kujitokeza kutokana na majanga kwani kwa sasa tumeshatoka kwenye hatua ya kusubiri kukabiliana na majanga na tupo katika hatua ya kuzuia na kujiandaa’’ amesisitiza Dkt. Manyata.

Aidha Manyata amewashauri wataalam wa serikali wanaosimamia utekelezaji wa miradi ya Mendeleo kuzishirikisha kamati za maafa ngazi za kata kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi hiyo ili ziweze kutoa ushauri na kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza iwapo miradi hiyo itatekelezwa katika maeneo yenye viashiria vya majanga yanayoweza kusababisha maafa.

Upande wake mshiriki wa semina hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Bugamba Kata ya Mwamgongo wilaya ya Kigoma Moshi Ahmad amesema mafunzo hayo yamewajengea uwezo katika kutambua viashiria na hatua za kuchukua kabla, wakati na muda mfupi baada ya kutokea kwa maafa.

‘’Naishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kushirikiana na mdau wa maendeleo Shirika la kimataifa la uhamiaji (IOM) Mkoa wa Kigoma kwa kufanikisha mafunzo yaliyotupa ujuzi huu kwani majanga yamekuwa yakitokea katika maeneo yetu na tukawa hatujui namna bora ya kuyakabili, lakini kwa sasa tumetambua nafasi na majukumu yetu katika kukabiliana na maafa’’ amesema Bugamba.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa