• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SERIKALI YAONYA WAVAMIZI WA ARDHI MAENEO YA TAASISI ZA DINI

Posted on: August 11th, 2022


Baadhi ya Watawa waliohudhuria kwenye  Ibada ya Jubilei ya Mhashamu Askofu Joseph P. Mlola  Mapadre na Watawa wengine iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Bikira Maria Mshindaji mjini Kigoma.

Mgeni Rasmi, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda akitoa neno mara baada ya Ibada ya  Jubilei ya Baba Askofu Mlola pamoja na watawa wengine iliyofanyika katika Kanisa la Bikira Maria Mshindaji jimboni Kigoma.


Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na  Uokoaji Thobias Andengenye, amesema Serikali haitosita kuwachukulia hatua watu wanaovunja Sheria kwa kuvamia Ardhi inayomilikiwa na Taasisi za kidini mkoani hapa.

Mkuu wa Mkoa ametoa Rai hiyo mara baada ya Ibada ya Maadhimisho ya Jubilei ya Askofu Joseph Mlola, Mapadre na  Watawa wengine iliyofanyika Katika Kanisa la Bikira Maria Mshindaji Jimbo la Kigoma, ambapo amemuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango.

Amesema Serikali kwa kushirikiana na wakuu wa Wilaya mkoani Kigoma wataendelea kushughulikia migogoro ya Ardhi na kuipunguza au kuimaliza kabisa kwani maeneo ya Taasisi za Dini yamepimwa na upatikanaji wake umefuata taratibu zote za kiserikali.

Akitoa neno neno la Shukurani, Mhashamu Askofu Mlola  amesema waumini waendelee kuwaombea ili wazidi kuimarika katika utumishi wa Mungu huku akisisitiza kuendelea kuimarika kwa Kanisa Katoliki mkoani Kigoma kufuatia kuongezeka kwa miito ya Kitawa na Mashirika ya kitume pamoja na ujenzi wa makanisa.

Pamoja na huduma zinazotolewa na Kanisa hilo Katika Mkoa wa Kigoma, amesema Kanisa linakabiliwa na changamoto ya uchakavu wa miundombinu ya Nyumba za Mapadre, Taasisi za Elimu na Afya, pamoja na uvamizi wa Ardhi katika maeneo yanayomilikiwa kihalali na Kanisa Katoliki mkoani hapa.

Mgeni Rasmi katika Jubilei hiyo, Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi kwa Mwaka 2022 na  Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anna Makinda amewapongeza Askofu Mlola na watawa wengine waliokuwa wakiadhimisha Jubilei hiyo ya Utumishi wa Mungu katika Kanisa.

Aidha amesisitiza wakazi kujitokeza na kutoa ushirikiano ili kufanikisha zoezi la Sensa ya watu na makazi huku akifafanua kuwa, zoezi hilo halitakamilika kwa siku moja hivyo watu watatatakiwa kuendelea kutoa taarifa pale watakapofikiwa na Makarani wa Sensa baada ya siku ya uzinduzi.

‘’Siku ya Sensa ya Watu na Makazi, kila mtu ahesabiwe kwenye kaya au eneo alikolala, Sote tuhakikishe tunahesabiwa ili kuipa nafasi Serikali kupanga na kutekeleza Mipango  kuendana na idadi yetu’’ amesema mama Makinda.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa