• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SERIKALI MKOANI KIGOMA KUSHIRIKIANA NA WADAU KUINUA KIWANGO CHA ELIMU

Posted on: July 4th, 2024

KATIBU TAWALA MKOA WA KIGOMA HASSAN RUGWA AKIZUNGUMZA NA  WADAU WANAOTEKELEZA MRADI WA SHULE BORA MKOANI KIGOMA( HAWAPO PICHANI) WALIPOTEMBELEA MKOANI HAPA KWA LENGO LA KUANGALIA MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MRADI HUO KATIKA MAENEO YA UJIFUNZAJI NA UFUNDISHAJI, USHIRIKIANO WA WALIMU NA WAZAZI(UWAWA) PAMOJA  NA  MAFUNZO ENDELEVU YA WALIMU KAZINI (MEWAKA)

Na. GLADNESS KUSAGA-KIGOMA.

Serikali mkoani Kigoma imeahidi kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa Elimu ikiwemo Mradi wa Shule Bora  ili kuboresha na kuimarisha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji ili kuendelea kuinua ubora wa Elimu.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa alipokutana na kuzungumza na wadau wa Elimu wanaotekeleza mradi wa Shule Bora  mkoani Kigoma na kusisitiza kuwa lengo la serikali ni kuona ubora wa Taaluma unaendelea kuimarika kutokana na maboresho ya Mazingira ya utoaji na upataji wa Elimu.

Amesema Serikali kupitia watendaji wa Sekta hiyo mkoani hapa wataendelea kushirikiana na wadau ili kupunguza changamoto zinazochangia kuzorotesha na kutofikiwa kwa malengo ya serikali katika utekelezaji wa mipango ya kitaaluma  sambamba na mdondoko wa wanafunzi.

Kiongozi wa Programu ya Shule Bora Taifa, Virginie Briand ameeleza kuwa mradi wa shule bora una lengo la kumuwezesha mwalimu kutekeleza majukumu yake kwa usahihi kupitia mafunzo wanayopatiwa sambamba na kusaidia zoezi la upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi wakiwa shuleni ili kufanikisha zoezi la ujifunzaji na ufundishaji.

Amesema kwamba vyumb vinavyotumika kutolea Elimu lazima viakisi picha halisi ya Mazingira ya ujifunzaji hali itakayopelekea kupunguza utoro na kuwafanya wanafunzi kuhudhuria vipindi madarasani bila kutoroka  na kuhakikisha walimu na wazazi wanasimamia zoezi la upatikanaji wa chakula  kwa watoto ili kuhakikisha watoto wanapata utulivu muda wa kujifunza.

Akizungumza na watendaji na wadau wa Sekta ya Elimu katika Kata ya Kidahwe, wilaya ya Kigoma, Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu Msingi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Susana Nussu amewataka wazazi kushirikiana na walimu kwa kufuatilia mahudhurio ya watoto na kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali kupitia miradi ya Elimu ya Kujitegemea (EK) iliyopo katika mazingira ya shule.

Bi. Susana amewakumbusha walimu mkoani Kigoma kujenga utamaduni wa kufanya Tathmini za mara kwa mara wakati wa ufundishaji na baada ya ufanyikaji wa mitihani ili kutambua maeneo yenye changamoto na mafanikio kisha kuchukua hatua ikiwemo kurudia mada, kutoa mazoezi ya kutosha kwa lengo la kuimarisha uelewa wa wanafunzi wao.

Aidha, Sasana amesema kuwa mbinu jumuishi za ufundushaji zitasaidia kukabiliana na changamoto ya utoshelevu wa walimu kwa ajili ya kufundisha baadhi ya masomo  na kuondoa pengo lililopo la kufikisha huduma za kitaaluma kwa wanafunzi.

Upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Matendo  Victor Gideon  amesemaa Mradi wa Shule Bora kupitia programu ya Ushirikiano wa Walimu na wazazi shuleni (UWAWA) imeleta mafanikio makubwa ikiwemo kuhamasisha wanafunzi kuhudhuria shule na kuongeza kiwango cha ufaulu kwa shule hiyo.

Amesema kupitia Programu ya Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini(MMEWAKA) pamoja na UWAWA, Shule ya Msingi Kidahwe ilipata jumla ya Shilingi 110,600,000 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vinne (4) vya Madarasa na matundu  matatu (3) ya vyoo, pamoja na walimu kupatiwa mafunzo kazi ili kuwajengea uwezo.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa