• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SERIKALI KUONDOA WAVAMIZI HIFADHI YA MAKERE KUSINI

Posted on: September 20th, 2022

Baadhi ya miche ya Miti aina ya misindano iikiwa imekauka baada ya kunyunyiziwa dawa  ya kukausha magugu na  wanaodaiwa kuwa ni wavamizi katika Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini. Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Thobias Andengenye (wa pili kushoto) akitazama Trekta   Mali ya Serikali lililochomwa moto na watu wanaodaiwa kuwa ni wavamizi katika Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini.Baadhi ya vitendea kazi vikiwa vimeungua.

Serikali mkoani Kigoma imeagiza kufanyika  kwa Operesheni Maalum ya Siku Ishirini na Moja kuanzia leo   Tarehe 20 Septemba 2022, ikiwa na lengo la kuondoa wavamizi wanaofanya shughuli za Kilimo na Ufugaji unaosababisha uharibifu wa mazingira Katika Msitu wa Hifadhi ya Makere Kusini uliopo wilayani Kasulu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Opersheni hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye amesema ni marufuku kwa mtu yeyote kuendelea na shughuli  za kibinaadamu katika eneo hilo ili lengo la Serikali kulifanya  kuwa Hifadhi liweze kutimia.

‘’Sheria za Uhifadhi wa Mazingira zinakataza kinachoendelea kufanyika katika eneo hili, hivyo nawatangazia watu wote kuwa hairuhusiwi kuendelea na shughuli za kilimo, ufugaji na nyinginezo   pia atakayekamatwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake’’ amesema Andengenye.

‘‘Naagiza yeyote atakayepata taarifa hii huku akiwa ndani ya mipaka ya hifadhi aondoke mara moja bila kusubiri kushurutishwa na Askari Maalum wa Doria ambao wataanza kuzunguukia maeneo  hayo mara baada ya kutolewa kwa tamko hilo.’’ Amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha amesikitishwa na uharibifu mkubwa wa vitendea kazi pamoja na miche ya Miti iliyokuwa ikiandaliwa  kwa ajili ya kupandwa katika eneo hilo la Hifadhi ili kukabiliana na uharibifu mkubwa wa mazingira uliofanywa na wavamizi hao.

Naye Mhifadhi Mkuu wa Mradi wa Shamba la Miti Makere Deograsian Kavishe amesema, watu wanaodhaniwa kuwa na uhusiano na wavamizi hao, walivamia Kambi ya Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania(TFS) iliyopo hifadhini humo na kuharibu vitendea kazi pamoja na miche ya Miti iliyokuwa imeoteshwa katika eneo hilo.

‘’Wavamizi walivamia  na kuteketeza mali mbalimbali ikiwemo kuchoma moto Hekta zaidi ya Mia moja za miti iliyopandwa, Trekta, Miche elfu tano ya miti aina ya Misindano, mashine za kusukuma Maji, matoroli pamoja na vifaa vingine vikiwa na  Thamani ya Shilingi  Milioni mia nne na hamsini.

Mhifadhi huyo amewataka wananchi kuheshimu Sheria za Nchi na kuzingatia maelekezo yanayotolewa na Serikali ili kuepuka uvunjifu wa Amani.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa