• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SERIKALI KUENDELEA KUSIMAMIA AFYA KWA WATUMISHI WA UMMA

Posted on: May 13th, 2024

NAIBU KATIBU MKUU OFISI YA RAIS MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA XAVIER DAUD AKISALIMIANA NA MKUU WA MKOA WA KIGOMA THOBIAS ANDENGENYE ALIPOWASILI MKOANI HAPA KWA AJILI YA KUFUNGUA KIKAO CHA ROBO YA TATU CHA KAMATI YA KITAIFA YA UKIMWI, VVU NA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA MAHALI PA KAZI KATIKA UTUMISHI WA UMMA.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi  wa Umma na Utawala bora Xavier Daud amesema serikali itaendelea kukabiliana na changamoto zinazohatarisha usalama wa Afya kwa Watumishi wa Umma ili na kuwawezesha kumudu kutoa huduma bora kwa wananchi.

Naibu Katibu Mkuu ametoa wito huo  alipozungumza wakati akifungua Kikao cha Robo ya Tatu cha Kamati ya kitaifa ya kudhibiti UKIMWI, VVU na Magonjwa yasiyoambukiza mahali pa kazi katika utumishi wa Umma, kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma na kusisitiza watendaji hao kudumisha usalama wa Afya zao ili waweze kumudu majukumu yao ya kiutendaji kazi Serikali.

‘’Kwa mwaka 2017 nchi ilikuwa na wagonjwa 688901 wenye magonjwa sugu yasiyoambukiza ambapo hadi kufikia mwaka 2022 kulikuwa na wagonjwa 1,456,881 ikiwa ni ongezeko la zaidi ya Asilimia hamsini, yakihusisha maradhi ya Shinikizo la damu, uzito uliozidi, Afya ya akili pamoja na kisukari’’ amesema Naibu Katibu Mkuu.

Amezitaja tabia na mienendo inayosabababisha ongezeko la magonjwa hayo kuwa ni pamoja na tabia bwete, kutozingatia taratibu za ulaji, matumizi ya vileo na kutokuzingatia ratiba ya ufanyaji mazoezi.

‘’Tumeendelea kutumia fedha nyingi kwa ajili ya kufanya matibabu badala ya kutumia gharama ndogo kwa ajili ya kujikinga na maradhi hayo, hali inayochangia kupoteza rasilimali fedha pamoja na muda mwingi kwa ajili ya kushughulikia matibabu’’ amesisitiza Daud.

Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema moja wapo ya changamoto kubwa kwa watumishi wa Umma ni suala la Afya ya Akili kutokana na wengi wao kukumbwa na hali ya msongo wa mawazo na kukosa wataalam wa masuala  hayo  katika Taasisi za Umma kwa ajili ya kuwasaidia kutatua changamoto hiyo.

''Kupitia kikao hiki wajumbe mnapaswa kutoka na maazimio yatakayoisaidia serikali kuona namna bora ya kutatua tatizo la Afya ya akili kwa watumishi wa Umma ili kuwanusuru na maamuzi wanayoweza kuyafanya wakiwa katika hali hiyo yanayoweza kuwaathiri wao wenyewe au wananchi wanaowahudumia'' amesema Rugwa.

Emma Lyimo, Mkurugenzi wa Utawala  na Usimamizi wa Rasilimali watu OR-TAMISEMI ambaye ni mjumbe wa kikao hicho amesema lengo la kikao ni kupata Taarifa za hali ya maambukizi ya UKIMWI, VVU na Magonjwa sugu yasiyoambikuza kutoka ngazi za Mamlaka za Serikali za Mitaa hadi Wizara.

Amesema taarifa zilizowasilishwa zinaonesha kuwa bado kunachangamoto kubwa katika muitikio wa watumishi wa Umma kujitokeza na kupima maradhi ya  UKIMWI,HIV na Magonjwa sugu yasiyoambukiza pamoja na kutokuwa tayari kuipokea elimu na kuwa tayari kudhibiti changamoto hizo.

‘’Watumishi wengi wa Umma hujikuta wakikaa ofisini muda mrefu, kula vyakula bila kuzingatia ratiba au makundi ya vyakula pamoja na kushindwa kufanya mazoezi jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa Afya zao’’ amesema.

‘’Watendaji katika Ofisi za Utumishi wahakikishe kunakuwepo na ratiba za watumsihi kushiriki michezo ikiwemo kufanya mazoezi ya viungo, kupima maendeleo ya hali za kiafya pamoja na kupunguza tabia za kushinda kazini badala ya kutumia muda wa ziada kushirki masuala ya kijamii’’ amesisitiza Lyimo.

Upande wake Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kigoma CPA Johson Gamba amesema Mazingira ya kazi ikiwemo uwepo wa mfululizo wa majukumu yameendelea kuwa changamoto na kisababishi kikubwa kwa wafanyakazi kukumbwa na maradhi sugu yasiyoambukiza.

‘’Nashauri serikali ifanye utafiti na ije na mapendekezo yatakayosaidia kubaini na kutoa miongozo itakayosaidia kubadili mitindo ya maisha ili kuendana na hali halisi ya mazingira ya kazi na  kuzikabili changamoto zitokanazo na magonjwa sugu yasiyoambukiza miongoni kwa watendaji wa Serikali’’ ameshauri Gamba.

Mratibu wa UKIMWI, VVU na Magonjwa yasiyoambukiza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Zabibu Mkamba amesema mpaka kufikia mwaka 2024 jumla ya watumishi 30  Wenye maradhi ya VVU na UKIMWI pamoja na 98 wenye magonjwa yasiyoambukiza wametambuliwa kupitia waratibu wa kiafya kutoka mamlaka ya Serikali za Mitaa na tayari wanaendelea kupatiwa huduma maalum za kiserikali.

Aidha kupitia kikao hicho, Mkamba amesema waratibu wa maradhi hayo wamepewa maelekezo ya kuhakikisha wanaendelea kuwatambua watumishi wenye changamoto hizo katika maeneo yao sambamba na kuendelea kutoa elimu na hamasa.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa