• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

WADAU WA AFYA WAKABIDHI MFUMO WA M-MAMA KWA SERIKALI KIGOMA

Posted on: August 21st, 2024

Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri za Wilaya za Wilaya Mkoani hapa wametakiwa kuongeza kasi ya uchangiaji fedha kwenye mfumo wa M-Mama sambamba na kuwalipa  Madereva Jamii wanaoendesha magari yanayotoa huduma hiyo ili kuwezesha zoezi la kuwafikisha wajawazito na watoto katika vituo  vya kutolea huduma za Afya kwa wakati.

Akizungumza kwenye kikao cha wadau cha kukabidhi Mfumo wa M-Mama kwa Serikali ya mkoa wa Kigoma, kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa wilaya ya Kigoma Salum Kalli amesema iwapo Halmashauri zitaupokea mfumo huo na kuzingatia miongozo ya uendeshaji wake  itasaidia kuendelea kupunguza vifo vya wanawake na watoto ili kudumisha uzazi salama.

Mhe. Kalli amesema watendaji hao kwa kushirikiana na wasimamizi wa mfumo wanapaswa kuimarisha uwajibikaji ili kuufanya mfumo huo kuwa endelevu na kutimza dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuhakikisha changamto ya vifo vya wajawazito, wanawake wanaojifungua pamoja na watoto inamalizika mkoani Kigoma.

Kupitia kikao hicho Mhe. Kalli amewahimiza wakazi mkoani hapa kuzingatia ulaji mlo kamili ili kulinda Afya zao dhidi ya maradhi yanayoweza kuzuilika kupitia ulaji wa chakula bora.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya amewataka wakazi mkoani hapa kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maradhi mbalimbali ikiwemo kuzingatia kaninu za Afya pamoja na namna bora ya kujikinga na magonjwa ya mlipuko.  

Upande wake mratibu wa Mfumo ngazi ya Mkoa Bernadetha Peter amesema,  jumla ya wateja 2,598 wamefanikiwa kusafirishwa ili kuvifikia vituo vya kutolea huduma ya Afya tangu kuanzishwa kwa mfumo huo mkoani Kigoma Aprili 20,2024 huku idadi ya wanawake ikiwa 2,220 na watoto 368.

Amesema mara baada ya mfumo kukabidhiwa serikalini, wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wanapaswa kuhakikisha Idara ya Fedha na Afya katika halmashauri zao zinasimamia uendeshaji wa mfumo kwa kuzingatia maelekezo yanayotolewa na seikali ili kufikia malengo yaliyowekwa.

Ameeleza kuwa, Mfadhili Mkuu wa Mradi Kampuni ya Vodafone kwa kushirikiana na wadau wanaotekeleza uendeshaji wa mfumo huo Shirika la Pathfinder International pamoja na Touch Health wanakabidhi rasmi mfumo huo katika mamlaka ya Mkoa hivyo Halmashauri zitapaswa kuendeleza majukumu ambayo wadau hao walikuwa wakiyatekeleza.

Ameyataja mambo ya kuzingatia ili halmashauri ziweze kufanikiwa katika utekelezaji  mpango huo kuwa ni pamoja na wafawidhi wa vituo kusimamia rufaa zote za mama na mtoto ili ziwe kwenye mfumo wa M-Mama, kuidhinisha malipo sahihi na kwa wakati kwa madereva Jamii pamoja na waganga wakuu na kamati za Afya wilaya kusimamia na kutoa taarifa kwa wakati.

‘’Nitoe rai kwa Uongozi wa Halmashauri kufanya malipo ya madereva kwa wakati sambamba na kuhakikisha gari za kusafirisha wagonjwa zinakuwa na mafuta ya kutosha ili ziweze kutumika muda wowote inapohitajika kufanyika hivyo’’ amesema Mratibu wa mfumo huo Bernadetha Peter.

Aidha ameyataja mafanikio ya mpango huo tangu ulipoanzishwa mkoani Kigoma kuwa ni pamoja na vituo vyote 291 kutumia Namba 115 wakati wa dharura ya mama na mtoto, uelewa wa jamii na wadau wote kuhusu umuhimu wa mfumo huona kuhakikisha unaimarika sambamba na kuendelea kufanyika kwa mawasiliano ya haraka miongoni mwa watumiaji wa mfumo.


Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa