• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

SAMIA APONGEZWA UJENZI SGR NA UBORESHAJI MIUNDOMBINU RELI YA KATI

Posted on: January 6th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mhe. Thobias Andengenye na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani Leo Januari 6, 2023 wamesafiri kwa Treni wakitumia mabehewa Mapya na ya kisasa yaliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya Reli ya kati na Kaskazini, kutoka Tabora hadi Kigoma kwa Lengo la kujionea hali halisi ya usafiri huo na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan  kwa ujenzi wa Reli ya Kisasa SGR baina ya Mikoa hiyo pamoja na kuendelea kuboresha miundombinu ya Usafirishaji katika reli hiyo.

Mara baada ya kufika Mkoani Kigoma wakuu hao walipata fursa ya kuzungumza na wananchi, viongozi wa Serikali, taasisi binafsi pamoja na wadau mbalimbali wa Maendeleo waliojitokeza kuupokea msafara huo, ambapo kwa pamoja walimpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kuidhinisha Fedha kiasi cha Shilingi Trilioni. 6.34 kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa SGR- awamu ya pili kipande cha Tabora-Kigoma  chenye urefu wa Kilomita 506.

Upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma  Thobias Andengenye amesema wananchi wanapaswa kutumia fursa ya ujenzi wa Miundombinu hiyo ya Reli kwa lengo la kujiimarisha kiuchumi kwa kuwa gharama za usafiri na usafirishaji wa bidhaa mbalimbali za kibiashara zitashuka na kufika kwa wakati.

Andengenye ameipongeza Serikali kwa kununua mabehewa mapya 22 ya kusafirisha abiria na kuwaasa wananchi kutumia usafiri wa treni kutokana na unafuu wa gharanma za nauli pamoja na   maboresho makubwa yanayoendelea kufanywa na Mhe rais katika miundombinu ya reli.

‘‘Nimesafiri kwa kutumia mabehewa haya na nimejionea mwenyewe ni mapya na yana hadhi ya kuitwa ya kisasa hivyo niwasihi mnapoyatumia  kusafiri mhakikishe mnayatunza ili yaweze kudumu na kurejesha fedha tulizowekeza’’ amesema Andengenye.

Amesema Rais Dkt. Samia ameendelea kuufungua mkoa wa Kigoma kwa kuboresha usafiri katika njia za Maji, kupanua Uwanja wa ndege, kujenga Barabara pamoja na kuimarisha mahusiano na nchi jirani za Congo na Burundi.

Naye Dkt. Buriani amesema wananchi waendelee kuwapuuza wanaobeza kazi nzuri zinazoendelea kutekelezwa na  Mhe. Rais Samia Suluhu kwani zinazidi kuliimarisha Taifa kiuchumi na kulifanya liweze kujitegemea .

‘‘Mikopo inayokopwa na  Serikali si chefuchefu bali ni mikopo yenye malengo ambayo kila mmoja wetu anaona matokeo yake, hivyo tunaendelea kumpongeza Mhe Rais  kwa kutafuta fedha kwa ajili ya kuliendeleza Taifa’’ amesema Buriani.

Katika Msafara huo, Viongozi hao wameambatana na Wenyeviti wa CCM(M) Tabora na Kigoma, Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Tabora, Katibu Tawala, Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Tabora, Viongozi Taasisi binafsi pamoja na waandishi wa Habari.

Pamoja na Safari hiyo, Kamati za Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kigoma na Tabora watakutana Januari 7, 2023 kwa ajili ya kufanya kikao cha Pamoja cha ujirani Mwema.

PICHA MBALIMBALI ZA MATUKIO YALIYOJIRI KATIKA SAFARI HIYO YA KUMPONGEZA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa