• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RITA KUZINDUA MPANGO WA USAJILI WATOTO CHINI YA MIAKA MITANO

Posted on: September 6th, 2023

Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini (RITA) unatarajia kuzindua mpango wa uhamasishaji wa usajili wa watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano bure ili waweze kupatiwa vyeti vya kuzaliwa.

Hayo yamebainishwa kupitia Semina ya Siku moja iliyofanyika mkoani hapa ikihusisha viongozi waandamizi wa Serikali wakiwemo Katibu Tawala Mkoa, Wakuu wa Wilaya, wataalam kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Kamati ya Usalama Mkoa, Makatibu Tawala wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Viongozi wa Dini pamoja na wazee Maarufu ikilenga kutumia nafasi zao kuhamasisha Jamii kushiriki kwenye zoezi hilo.

Naibu Kabidhi Mkuu wa Serikali RITA, Irene Lesulie amesema kuwa mpango huo unalenga kubaini, kusajili na kutoa vyeti kwa watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano waliozaliwa  nchini kufuatia uwepo wa idadi ndogo ya waliosajiliwa na kupewa vyeti ikilinganishwa na idadi halisi ya watoto waliozaliwa.


‘’Kwa mwaka 2022 jumla ya watoto 442,662 walizaliwa mkoani Kigoma ambapo kati yao ni watoto 46,480 walisajiliwa na kupatiwa vyeti ikiwa ni sawa na Asilimia 10 ya watoto waliozaliwa mwaka huo’’ amesema Lesulie.

Amesema zoezi la usajili na utoaji wa vyeti limekuwa likisuasua na kusababisha idadi ya wanaosajiliwa ili kupata vyeti kuwa ndogo hivyo mpango huu umelenga kufanya uhamasishaji ili kuongeza idadi ya watoto watakaosajiliwa na kupata vyeti kwa kuwasogezea karibu huduma kupitia vituo vya kutolea huduma za Afya na Ofisi za watendaji wa kata.

Akizungumza wakati wa akifungua Semina hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Michael Masala amesema mpango huo utatoa fursa kwa Serikali kupata taswira ya hali halisi ya mahitaji ya kundi hilo pamoja na kupanga mipango ya Maendeleo mkoani Kigoma.

Masala amewataka watendaji wa Serikali wanaosimamia utekelezaji wa zoezi hilo kuhakikisha taratibu za upekuzi na utambuzi wa wanaostahili kupatiwa vyeti hivyo zinazingatiwa na kutekelezwa kwa ufanisi.

Pamoja na hilo, Kanali Masala amesema zoezi hilo halina uhusiano wowote na utoaji wa Uraia wa Tanzania na wale wenye uhitaji huo wahakikishe wanazingatia taratibu rasmi zilizowekwa na Serikali.

Upande wake mwakilishi kutoka OR-TAMISEMI Mariam Mkumbwa amewataka watendaji wanaosimamia zoezi hilo kuhakikisha taarifa zote zinazokusanywa zinaingizwa kwenye mfumo ili mara baada ya usajili taarifa za watoto hao ziweze kusomeka kwenye mifumo mingine ya kiserikali.

 Mpango wa usajili kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano ulianza mwaka 2013 ambapo hadi kufikia Mwaka 2023, jumla ya watoto Milioni 8.6 wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa