• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

REA YAENDELEA NA MIKAKATI KUUNG'ARISHA MKOA WA KIGOMA

Posted on: November 30th, 2022

Wakala wa Nishati Vijijini ulianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 8 ya Mwaka 2005 kwa lengo la kuhamasisha upatikanaji wa Huduma Bora ya Umeme katika maeneo yote ya vijijini huku ukiwa na dhamira ya kutoa huduma ya kisasa ya Usambazaji wa nishati rahisi na salama, kwa ufanisi huku ikiwa rafiki kwa Mazingira.

 Dhamira ya Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ni kuhakikisha  huduma hiyo muhimu inawafikia watanzania wote Tanzania Bara katika maeneo ya vijijini.

Mkoa wa Kigoma umeendelea kunufaika na huduma za REA, ambapo wilaya zote sita(6) za mkoa zimefikiwa kwa kiwango tofauti, ambapo hadi kufikia Septemba 2022 jumla ya Vitongoji 883 kati ya 1,855 vimekwisha kuunganishwa na miundombinu ya huduma hiyo.

Wakala huo umeendelea kutekeleza miradi  ya kupeleka Umeme katika Wilaya za Kasulu, Kigoma vijijini, Buhigwe, Kibondo, Uvinza na Kakonko kupitia awamu mbalimbali kwa kuzingatia hali ya upatikanaji wa Fedha kuendana hali ya bajeti, japo baadhi ya maeneo miradi imekuwa ikichelewa kiutekelezaji kutokana na changamoto za watendaji pamoja na upatikanaji wa vifaa.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy anasema kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 mradi wa REA Awamu ya Tatu  Mzunguuko wa Pili  ulianza kutekelezwa  Mwezi Aprili 2022 chini ya Mkandarasi Mzawa State Electrical and Technical Service wenye Thamani ya Shilingi Bilioni 47,176,369,574.58 ukilenga kupeleka  umeme katika vijiji 89 kwa wilaya sita za mkoa.

Mradi huo unatarajiwa kukamilika  Oktoba 2022, ambapo mpaka sasa mkandarasi yupo kazini na kazi zilizokamilika ni usanifu wa michoro kwa wilaya zote sita, uandaaji wa njia za umeme pamoja na uchimbaji wa mashimo ya nguzo, kazi zinazoendelea katika wilaya za Kasulu, Buhigwe, Kigoma Vijijini na Kakonko.

Mha. Hamisi anasema mradi mwingine unaotekelezwa ni REA Awamu ya Tatu Mzunguuko wa Kwanza  wenye Thamani ya Shilingi Bilioni 13,315,362,802.32 unaotekelezwa na Mkandarasi M/S TANESCO kupitia Kampuni Tanzu ya ETDCO, unaendelea huku malengo ikiwa ni kufikisha nishati hiyo muhimu katika vijiji 69 vya Wilaya za Kakonko na Kibondo.

Anasema kupitia mradi huu, vinini 25 kati ya 29 vimeunganishwa na Umeme katika wilaya ya Kakonko  huku vijiji 31 kati ya 40 vikiunganishwa kwa wilaya ya Kibondo ambapo hadi kufikia mwezi Disemba 2022 vijiji 13 vilivyosalia kwa wilaya zote mbili vitakua vimeunganishwa na huduma hiyo.

Utekelezaji wa Mradi wa Awamu ya Tatu Mzunguuko wa Kwanza unaotekelezwa na Mkandarasi M/S CCCE Etern ulioidhinishiwa Shilingi Bilioni 38,623,349,313.29 umekamilika huku vijiji 87 vikiwa vimeunganishwa na miundombinu ya Umeme katika  wilaya za Kasulu, Uvinza, Buhigwe na  Kigoma vijijini.

Mha. Hamisi anasema, licha ya utekelezaji wa kazi hizo za kuunganisha Nishati hiyo muhimu kwa maendeleo ya wanakigoma, maeneo mengi ya vitongoji bado hayajafikiwa kutokana na baadhi kuwa katika hatua za uhakiki, kutofikiwa na awamu za utekelezaji pamoja na utayari wa Bajeti katika kuyalenga maeneo hayo.

Aidha ametaja sababu nyingine  zinazosababisha kutofikiwa kwa malengo yanayowekwa katika mikataba kuwa ni kasi ndogo ya wakandarasi katika kutekeleza miradi, changamoto ya upatikanaji wa vifaa kwa wakati pamoja na baadhi ya wananchi kuhujumu miundombinu ya umeme inayoendelea kuwekwa.

Mhandisi Hamisi amezitaja hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa katika kukabiliana na changamoto hizo  ikiwemo baadhi ya wakandarasi wanoshindwa kutekeleza miradi yao kwa wakati kupewa onyo au kusitishiwa mikataba yao ya kazi na kupewa wakandarasi wengine. Aidha wamekuwa wakiikabili changamoto ya kupanda kwa bei za vifaa kwa kupitia upya mikataba na kurekebisha bei kuendana na hali ya soko la vifaa.

Katika kuhakikisha ulinzi  na usalama wa miundombinu ya umeme, REA inaendelea kutoa Elimu na Hamasa ya utunzaji miundombinu hiyo kwa maslahi mapana ya watanzania wote huku wakiahidi kupeleka umeme katika vitongoji vyote  972 vya Mkoa wa Kigoma ambavyo havijafikiwa na huduma hiyo muhimu kutegemea hali ya upatikanaji wa Fedha.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DCP NARCIS MISSAMA AFANYA ZIARA MKOANI KIGOMA

    May 07, 2025
  • JAJI ASINA AKAGUA ZOEZI LA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI-KIGOMA

    May 03, 2025
  • VYAMA VYA WAFANYAKAZI VISIGEUKE MAHAKAMA ZA KUWAHUKUMU WATUMISHI-RC ANDENGENYE

    May 01, 2025
  • PICHA; MAENDELEO YA UJENZI WA UKUMBI WA DKT. PHILIP MPANGO KATIKA OFISI YA MKUU WA MKOA WA KIGOMA

    April 30, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa