• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko / Mrejesho |
KIGOMA   REGION
KIGOMA   REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Seksheni ya Elimu
      • Seksheni ya Afya
      • Seksheni ya Miundombinu
      • Seksheni ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Mipango na Uratibu
      • Seksheni ya Uchumi na Uzalishaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Fedha
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwami
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Kibondo
      • Halmashauri ya Kibondo
    • Wilaya ya Kigoma
      • Halmashauri ya Kigoma
      • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Wilaya ya Kakonko
      • Halmashauri ya Kakonko
    • Wilaya ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu
      • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Wilaya ya Uvinza
      • Halmashauri ya Uvinza
    • Wilaya ya Buhigwe
      • Halmashauri ya Buhigwe
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Kigoma Ujiji
    • Halmashauri ya Buhigwe
    • Halmashauri ya Kasulu
    • Halmashauri ya Kasulu Mji
    • Halmashauri ya Kibondo
    • Halmashauri ya Uvinza
    • Halmashauri ya Kakonko
    • Halmashauri ya Kigoma
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Kigoma Special Economic Zone
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mikakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Picha

RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

Posted on: May 27th, 2025


MKUU WA MKOA WA KIGOMA CGF(Rtd) THOBIAS ANDENGENYE AKIWASILI KATIKA UWANJA WA ZAHANATI YA RUSIMBI NA KUPOKELEWA NA MKUU  KATIBU TAWALA MKOA MHE. HASSAN RUGWA  KABLA YA KUZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI WA VYANDARUA KWA MKOA WA KIGOMA.

MKUU WA MKOA WA KIGOMA(KUSHOTO) AKITETA JAMBO NA KATIBU TAWALA MKOA MHE. HASSAN RUGWA WAKIWA KWENYE HAFLA FUPI YA KUZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI WA VYANDARUA KIMKOA LILILOFANYIKA KATIKA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI

MKUU WA MKOA WA KIGOMA MHE. THOBIAS ANDENGENYE AKIKATA UTEPE KUASHIRIA UZINDUZI RASMI WA ZOEZI LA UGAWAJI WA VYANDARUA KIMKOA.

Jumla ya kaya 503,762 zinatarajiwa kunufaika na mpango wa ugawaji wa vyandarua 1,775,359 vinavyotolewa na Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Afya ikiwa ni utekelezaji Mpango wa Taifa wa kudhibiti Maralia (NMCP) ambapo  Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa yenye kiwango kikubwa cha maambukizi.

Akizindua rasmi zoezi la ugawaji wa vyandarua hivyo kupitia hafla fupi iliyofanyika katika Zahanati
ya Mtaa wa Rusindi Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amesema  kwa mujibu wa taarifa zinazotolewa kupitia mfumo wa kutolea taarifa za wagonjwa (TDHS), kwa mwaka 2024 jumla ya wagonjwa 309,080 walibainika na maambukizi ya ugonjwa huo kimkoa, ambapo idadi ya vifo ilikuwa watu  264 vikihusisha watoto 177 na watu wazima 87.

MKUU WA MKOA WA KIGOMA MHE. THOBIAS ANDENGENYE MARA BAADA YA KUKATA UTEPE KUASHIRIA KUZINDULIWA RASMI KWA ZOEZI LA UGAWAJI WA VYANDARUA MKOANI KIGOMA

Amesema vyandarua hivyo vinatolewa bure na serikali hivyo wasimamizi wanapaswa kusimamia vizuri zoezi la ugawaji  ili viwafikie walengwa huku akitoa wito kwa wanufaika kufanya matumizi sahihi ili viweze kuleta tija katika kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa maralia mkoani Kigoma na nchini kwa ujumla.

Aidha amewataka  walengwa katika halmashauri zote nane za mkoa ambao watanufaika na mgao huo kuvitumia vyandarua hivyo kwa usahihi na kuachana na dhana potofu kuwa matumizi yake yanaweza kuchangia kupunguza nguvu za kiume au kusababisha changamoto za uzazi kwa wanawake.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa amesema zoezi la ugawaji wa vyandarua hivyo litazigusa kaya zote mkoani Kigoma.

Amesema wakazi wa Kigoma  wameendelea kuwa mashuhuda kwa ⁰kujionea namna serikali ya awamu ya sita inavyoendelea kuwagusa wananchi kupitia uboreshaji mkubwa katika utoaji wa huduma za Afya nchini.

Victor Sungusia, Afisa Ugavi MSD  amewataka wananchi kutumia vyandarua hivyo kwa lengo la kujikinga na maralia ili kutumia muda wao katika kufanya kazi za maendeleo badala ya kushinda wakisguhulikia changamoto za kiafya zitokanazo na maradhi hayo.

Amesema vyandarua hivyo  vitatoelewa kwa kila kaya ambao kupitia mpango huo  maeneo yote ya mkoa yatafikiwa.

Matangazo

  • MAZOEZI KWA AFYA YAKO March 23, 2017
  • UCHAGUZI WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 September 12, 2024
  • UJIO WA MADAKTARI BINGWA MKOANI KIGOMA November 12, 2018
  • Fomu ya Usajili wa Maonesho TBS Kigoma May 01, 2022
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • RC ANDENGENYE AZINDUA RASMI ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA KIMKOA

    May 27, 2025
  • JAMII INAPASWA KUZINGATIA CHANJO KUJILINDA NA MARADHI

    May 20, 2025
  • MRADI WA UHIFADHI MAZINGIRA WAZINDULIWA KIGOMA

    May 15, 2025
  • RC ANDENGENYE AKABIDHI VITENGO VITENGO VYA LISHE MKOA NA WILAYA UVINZA

    May 09, 2025
  • Ona vyote

Video

RC ahimiza wananchi anuani za Makazi
Video nyingine

Tovuti zinazo fanana

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BUHIGWE
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KAKONKO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
  • HALMASHAURI YA MJI KASULU
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIBONDO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA
  • HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

Tovuti zinazo husiana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI PORTAL
  • IKULU
  • OFISI YA TAKWIMU YA TAIFA
  • IDARA YA HABARI MAELEZO
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    MKOA WA KIGOMA

    Anuani: S.L.P 125

    Simu: 0282802330

    Simu ya kiganjani: +255766853404

    Barua Pepe: ras@kigoma.go.tz / ras.kigoma@tamisemi.go.tz / info@kigoma.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

https://bachelorthesiswritingservice.com

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Kigoma. Haki zote zimehifadhiwa